Wednesday, July 18, 2007

Jaji Mkuu mpya huyu



RAIS Jakaya Kikwete amemteua Jaji Augustino Ramadhan kuwa Jaji Mkuu wa nne wa Tanzania, baada ya Jaji Mkuu Barnabas Samatta kustaafu rasmi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo jana, uteuzi wa Jaji Ramadhan ambaye ni Jaji wa Mahakama ya Rufani kwa muda mrefu sasa, unaanza mara moja.

Taarifa hiyo ilielezea kuwa Jaji Ramadhani ataapishwa kesho jioni Ikulu jijini Dar es Salaam.

Jaji Ramadhani ambaye ni mwenye vipaji vingi, kabla ya kuingia katika shughuli za mahakama, alikuwa katika jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) akifanya kazi huko katika Idara ya Sheria na alitoka jeshini akiwa na cheo cha Brigedia Jenerali.

Pia amewahi kuwa Jaji katika Mahakama ya Afrika Mashariki ambako alikuwa yeye pamoja na Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania, Jaji Joseph Warioba, walikuwa wakiiwakilisha Tanzania.

Kwa upande wake, Kenya ilikuwa ikiwakilishwa na Jaji Moijo ole Keiwu na Jaji Kassanga Mulwa walioteuliwa na Rais wa zamani wa Kenya, Daniel arap Moi.

Kwa Uganda walikuwapo majaji Joseph Mulenga na Jaji Solony Bosse, aliyepata kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki.

Sambamba na hilo, Jaji Ramadhan pia ni mpiga kinanda maarufu katika kwaya ya wa Kanisa la Anglikana jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa juzi kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), ilisema kuwa Mahakama ya Tanzania itafanya kikao maalum cha kumuaga kitaaluma Jaji Msataafu Samatta, ambacho kitafanyika Julai 19, mwaka huu kwenye jengo la Mahakama ya Rufani iliyopo Kivukoni Front.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Jaji Samatta atastaafu ifikapo Julai 20, mwaka huu. Katika shughuli za kumuaga, atakagua gwaride la heshima mbele ya jengo hilo.

Miongoni mwa watu watakaohudhuria siku hiyo ni Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Mary Nagu akiwemo Naibu wake, Mathias Chikawe, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika ambaye atatoa hotuba.

Mbali na Jaji Samatta, Watanzania wengine wazalendo waliowahi kushikilia nafasi ya Jaji Mkuu ni Augustino Saidi na Francis Nyalali.

Hii ina maana kwamba Jaji Ramadhan anakuwa pia Mzanzibari wa kwanza kushika wadhifa wa juu katika duru za mahakama nchini Tanzania. Unaweza kumsoma zaidi katika gazeti la Mwananchi

2 comments:

Simon Kitururu said...

Hongera Jaji!Jina lake lime wachanganya wadau waendekeza dini.Mtandaoni nimeshakuta majadiliano ya Wakristo wamlalamikiao Raisi kuwa anaendeleza kuleta Waislamu na Waislamu walalamikao kwanini cheo hicho hajawahi kupewa Muislamu.Duh!

Anonymous said...

[url=http://is.gd/Bp1q3L][img]http://stomsk.ru/pics/spymobile.ol1[/img][/url]
[url=http://archive.org/details/trankascheckdu/]Cars 2 Spy Shifters Finn Mcmissile[/url] [url=http://beaufortteaparty.webs.com/apps/profile/109034678/]Can You Read Text Messages Online From T Mobile [/url] [url=http://archive.org/details/quiresadle/]Trace A Cell Phone Location For Free[/url] http://vampiretheory.webs.com/apps/profile/109034678/ spy kids 3d game over intercept text messages online for free monitoring cell phone location nokia 5233 spy call software free download cell phone spy software locate a cell phone by number for free spy optics women s cosmik sunglasses
Phone Tracker Free
Boost Mobile Phone Store Locator
Cell Phone Spy App Reviews
http://www.sjcbridges.org/about-us/our-staff/ free cell spy software downloads phone tracker online spy camera android apk
[url=http://archive.org/details/suppwesdetab/] Spy Vs Spy Book 1 [/url] [url=http://archive.org/details/piebedvema/] Monitor Mobile Phone Free [/url] http://gmolabeling.webs.com/apps/profile/109034678/ watch himym online free season 7 episode 1 spy gear toys r us uk gps cell phone tracker app android spy kids 2011 rotten tomatoes gps tracking devices cars spy cell phone spying free trial wireless spy gsm sim phone device surveillance ear bug