Friday, April 28, 2006
Kijiji cha Mwananchi kimewaka moto
Haya tena wanablogu wenzangu kumekucha tena safari hii nawaleteeni wanablogu wawili matata kweli kweli. Wa kwanza huyu ni bosi wangu katika masuala ya spoti afahamika sana kama Angetile Osiah au Mzee wa Ujerumani, amebobea katika fani hii wengine hupenda kumwita kisima cha fikra michezoni, nadhani hata kuwa mgeni kwenu waweza kumtembelea kwa kubofya hapa. Na mwingine ni mwanamama huyu, Mzanzibari ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii, ni hazina tosha ya fikra za kisiasa na kijamii, aweza kukusisimua kwa kuipata vyema historia ya Zanzibar na maeneo mengine, jinale Hawra Shamte, waweza kumpata kwa kubonya hapa. Haya mambo yanazidi kuwa mambo bloguni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RC CHALAMILA ATOA SIKU SABA KWA MUAFAKA WA MGOGORO WA ARDHI TOANGOMA
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, ametoa muda wa siku saba kwa wadau wanaohusika na mgogoro wa muda mrefu wa ardhi katik...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...
3 comments:
Poa sana kaka kwa kutuletea "hivyo Vichwa" bloguni
Yahya lazima nikuletee zawadi ya tende maana unanivalisha nguo sasa kila nipitapo.
Mzee wa mshitu naona Waziri wa Teknolojia (MK) kashakutembelea. Huyu bwana achana naye anajenga nyumba za Tanzania akiwa UK, "Kinana apewe sifa' Amen
Post a Comment