hebu cheki watoto hawa walivyo bize na kilimo, halafu unambie kuwa eti hawa watavuna cha kutosha kulisha wananchi wote, hivi kweli jamani tutafika wakati kilimo ndo kinachangia asilimia zaidi ya 75 ya ajira za wabongo.
Wednesday, October 03, 2007
Watoto na kilimo
hebu cheki watoto hawa walivyo bize na kilimo, halafu unambie kuwa eti hawa watavuna cha kutosha kulisha wananchi wote, hivi kweli jamani tutafika wakati kilimo ndo kinachangia asilimia zaidi ya 75 ya ajira za wabongo.
Tuesday, October 02, 2007
shambani kwetu
Makatibu wakuu 15 kutembelea Buzwagi
*Hazina ya dhahabu Tulawaka ukingoni
Na Mwandishi Wetu wa Mwananchi
MAKATIBU wakuu kutoka wizara 15 wanatarajiwa kuanza ziara ya kutembelea migodi ya dhahabu Buzwagi, North Mara, Bulyanhulu na Tulawaka ambayo inamilikiwa na Barrick ili kuona shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo.
Akizungumza na Mwananchi, Afisa Mwandamizi wa Mawasiliano wa Barrick Tanzania, Teweli Teweli alisema lengo la ziara hiyo ni kuelimisha wadau mbalimbali kuhusiana na sekta ya madini.
"Ziara hiyo ni mpango wa Barrick ambao una lengo la kuelimisha wadau mbalimbali wakiwamo waandishi wa habari, viongozi wa serikali kuhusiana na sekta ya madini, watu wengi bado hawajui mambo mengi ya sekta hii mpya Tanzania," alisema.
Tayari Kampuni ya Barrick imeshapeleka baadhi ya wahariri wa habari kutembea mgodi wa Bulyanhulu na Tulawaka mwishoni mwa wiki iliyopita kwa dhumuni hilo. Wahariri hao ni kutoka magazeti ya Mtanzania, This Day, Mwananchi na kutoka Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
Ratiba ya safari hiyo inaonyesha kwamba makatibu wakuu hao wataondoka jijini Dar es Salaam Jumamosi alfajiri na kuwasili Bulyanhulu saa tatu asubuhi na kupata maelezo mafupi kisha kwenda kwenye ndani ya mgodi kuangalia shughuli za uchimbaji madini zinavyoendelea. Siku hiyo pia watatembelea shughuli za maendeleo ambazo mgodi huo unafanya kwa wanakijiji wanaozunguka maeneo hayo.
Siku ya pili, ratiba inaonyesha kwamba makatibu hao wakuu watakwenda katika mgodi wa Tulawaka ulioko mkoani Kagera katika wilaya ya Biharamulo kwa ajili ya kutembea sehemu za machimbo na kuangalia programu ya utunzaji mazingira katika eneo hilo. Siku hiyo wataenda katika mgodi wa North Mara na Buzwagi kwa ajili ya shughuli za kukagua mgodi.
Wakati huo huo, mgodi wa Tulawaka ambao ulianza uzalishaji 2005 unatarajia kumaliza hazina yake ya madini ya dhahabu 2010 ikiwa ni miaka miwili imebakia sasa.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Talawaka, Scott Artkinson aliwaambia waandishi wa habari waliotembelea mgodi huo mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba hazina ya madini katika mgodi huo inatarajia kuisha miaka miwili ijayo na hivyo kama hawatagundua hazina zaidi, mgodi huo utafungwa.
"Mgodi utakamilisha shughuli zake 2010, lakini tunaweza kugundua hazina ya madini wakati tukiendelea na uchimbaji," alisema.
Tofauti na migodi mingine inayomilikiwa na Barrick, Mgodi wa Tulawaka unatoa dhahabu tu na kiwango chake cha ubora ni kikubwa. "Kuanzia mwaka jana, tumeanza kupata faida, kwa hiyo mgodi wetu unajiendesha kwa faida," alisema
Artkinson alisema kwamba mwaka jana mgodi ulipata faida ya Sh9 bilioni na mwaka huu wanatarajia kupata faida ya Sh13bilioni.
Monday, October 01, 2007
Ugeni wa WTO
MAKAMU wa Rais, Dk Ali Mohamed Shein, amesema misaada ya kifedha inayotolewa na wahisani kwa nchi zinazoendelea kwa ajili ya kuimarisha biashara isiwekewa masharti mazito ili kusaidia kukuza sekta hiyo katika nchi za kiafrika.
Dk Shein alisema hayo jana kwenye mkutano wa majadiliano ya jinsi ya kukusanya fedha kwa ajili ya misaada ya kimandeleo unaofanyika jijini Dar es Salaam, ambao umeandaliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (ADB), Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi kwa Afrika na Shirika la Biashara Duniani (WTO) kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.
Alisema fedha hizo zinatakiwa pia kutolea kama msaada na siyo mikopo ili kuziwezesha nchi zinazopokea kufanikisha malengo yake katika kukuza biashara.
“Misaada ya kifedha kutoka kwa wahisani (AFT) inatakiwa kuwa ya uhakika na ipatikane kirahisi na kwa wakati badala ya kuwa na mlolongo mrefu unaombatana na mambo ya kisiasa, alisema Dk Shein.
Lengo la mjadala huo ni kuzihamasishga serikali, wafadhili na sekta binafsi kutoa changamoto sahihi kwa bara hili na kuweka bayana mahitaji na kushirikisha utatuzi wa matatizo na changamoto za kibiashara.
“Misaada yakifedha inayotolewa kwa ajili ya maendeleo lazima ilingane na mahitaji halisi ya walengwa,” alisitiza Dk Shein, kuongeza kuwa katika hilo kunahitajika kuwepo kwa mawasiliano sahihi na wapokeaji wa misaada hiyo iliiweze kuwa na manufaa wahusika.
Air Tanzania
Subscribe to:
Posts (Atom)
Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma
Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya mazungumzo na Fitch Ratings Ltd amb...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...



