Thursday, September 03, 2009

Chadema wazindua mkutano kwa kishindo




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) leo kimeanza mkutano wake mkuu utakaoendelea hadi kesho kumchagua Mwenyekiti wake wa taifa ambapo pia kimezindua programu ya kusajili wanachama kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu ijulikanayo kama ‘Electronic Membership’.(Cheki wanachama hapo juu pichani walivyocharuka).

Mbali na uzinduzi wa utaratibu huo ambao ni wa kwanza barani Afrika, chama hicho pia kimezindua vitabu viwili, “Programu ya Chadema ni Msingi” na “Programu ya Mafunzo ya Wanachama na Viongozi”.

Vitabu hivyo vinalenga kuwa na mwongozo mmoja kwa viongozi wote wa chama hicho nchini.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mbezi Beach, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema usajili wa wanachama kwa njia ya simu, una lengo la kukusanya wanachama milioni moja kabla ya kuisha kwa mwaka huu.

“Gharama ya kutuma ujumbe mfupi itakuwa ni Sh300 kwa ujumbe wa simu, fedha ambazo zitaweza kuwasaidia wabunge na madiwani wetu. Hatutaki kuwa na viongozi ambao wanatumia fedha zao kwa ajili ya kuwawezesha kwenye kampeni na shughuli mbalimbali za chama,” alisema Mbowe.
Alisema utaratibu wa kuwa na matawi ya wanachama umepitwa na wakati kwani matawi hayo siku hizi yamegeuzwa kuwa vijiwe vya uhalifu.

“Mashina ya wakereketwa siku hizi yamekuwa vijiwe vya wahalifu. CCM wanatakiwa watambue kwamba programu hii haiwezi kuundiwa zengwe na wakitufuata huku watakuwa na sababu zao. Lakini wao pia wajifunze kuachana na matawi kwani nchi nyingi kama Kenya na Marekani wameshaachana na mtindo wa matawi,” alisema Mbowe
Habari ya Mussa Mkama na Fidelis Butahe, Picha na Venance Nestory

Kipanya leo

ABRAMOVICH KUPANDA KILIMANJARO




MMILIKI wa Klabu ya soka ya Chelsea, inayoshiriki katika ligi kuu ya Uingereza, Roman Abramovich ametua mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kupanda Mlima Kilimanjaro.
Abramovich, ambaye ni tajiri wa Kirusi atakuwepo nchini hadi Septemba 11, mwaka huu atakapoondoka kurudi Uingereza anakoishi.
Tajiri huyo wa klabu ya Chelsea alikuja jana saa 1 jioni akiwa na watu 6 na amefikia katika Hoteli ya River Trees Country Inn, iliyopo eneo la USA River nje kidogo ya Mji wa Arusha ambayo hivi sasa haruhusiwi mtu mwingine kuingia katika hoteli hiyo.
Meneja wa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ,Said Mzava jana jioni alisema Abramovic amefurahi kufika Tanzania kuona mlima Kilimanjoro na vivutio vingine vya utalii.
Huku akiwa analindwa na walinzi watatu, Abramovich alikataa kuzungumza na vyombo vya habari akisema kuwa amechoka anahitaji kupumzika.
Abramovich ambaye amekuja na ndege yake binafsi aina ya Boeing 767, pia alikutana na kusalimiana na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara nchini, Cyril Chami aliyekuwepo uwanjani hapo kwa shughuli zake binafsi.

Wednesday, September 02, 2009

Pinda Atua Kenya



Waziri Mkuu,Mizengo Pinda na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga wakitazama ngoma baada ya Waziri Mkuu Pinda kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta kwa ziara ya siku mbili.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

RAIS JAKAYA AKIBADILISHANA MAWAZO NA RAIS MUAMAR GADAFI!


Rais Jakaya Kikwete akiongea na mwenyeji wake Kiongozi wa Libya Muamar Gadafi ambaye pia amesherehekea miaka 40 ya utawala wake hivi karibuni rais pia alihudhuria mkutano wa AU nchini Libya.

Zain yajiunga mkongo wa mawasiliano na Seacom


Zain Tanzania imekuwa kampuni ya kwanza ya simu za mkononi kujiunga na mkonga wa baharini wa kimataifa ambao utaiwezesha Tanzania na eneo la Afrika Mashariki kupata huduma za data za kasi zaidi na yenye gharama nafuu.

SEACOM ina uwezo mkubwa wa kubeba na kuunganisha huduma za sauti na data ukilinganisha na mfumo wa satellite uliozoeleka. ‘’Wateja wetu watarajie kupata huduma za kasi zaidi za intaneti, huduma bora zaidi za simu za sauti, kasi katika kuunganishwa na uwezo mkubwa wa kupokea huduma za data,’’ alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania.

‘’Uhusiano wa moja kwa moja wa huduma ya Zain ya 3.5G na SEACOM itawawezesha wateja wetu kupata huduma ya kasi ya intaneti kupitia simu za mkononi na uwezo mkubwa wa kupokea data kutoka vituo vikuu vya data duniani.

Hii ni hatua ya maendeleo kwa Zain na tunajivuna kwamba tunaendelea kuweka historia nchini Tanzania kwa kuwa kampuni ya kwanza ya simu za mkononi kuleta huduma hii iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu, na yakutegemewa kwa wateja wetu, sekta ya biashara na taasisi za elimu,’’ alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania.

Mkonga huu ni wa kwanza katika miradi ya mikonga ya baharini Afrika Mashariki ambao utaiunganisha Tanzania na dunia, Licha ya maendeleo katika sekta ya habari na mawasiliano ya teknolojia Afrika katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, bara la Afrika bado lina matumizi madogo ya simu na intaneti.

Maendeleo ya kiuchumi Afrika Mashariki na Afrika Kusini pia yamecheleweshwa na bei kubwa ya teknolojia ya mawasiliano na habari na miundo mbinu hafifu ya mawasiliano. Mahitaji ya huduma za data katika bara la Afrika yamekuwa yakizidi huduma iliyopo kwa sasa, na mkonga utasaidi kukuza biashara nchini Tanzania na katika bara hili, alisema Khaled.

Tuesday, September 01, 2009

Mramba huyooo



KESI ya matumizi mabaya ya ofisi yaliyoisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni inayowakabili mawaziri wa zamani Basil Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu wa wizara ya Fedha na Uchumi Gray Mgonja inatarajiwa kuendelea kusikilizwa kwa awali Septemba 16 mwaka huu.

Hayo yalielezwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Hakimu Mkazi Eva Nkya wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Mara ya mwisho kesi hiyo ililazimika kuahirishwa baada ya kuharibika kwa kompyuta iliyokuwa ikirekodi mwenendo mzima wa kesi hiyo.

Washitakiwa hao wanadaiwa kuwa wakiwa waajiriwa wa serikali walitumia madaraka yao vibaya kwa kuipatia msamaha wa kodi kampuni ya M/S Alex Stewart na kuisababishia hasara serikali ya kiasi hicho cha pesa.

MTUHUMIWA WA “KUFUTA MADENI” YA MIKOPO AKIRI KOSA, AHUKUMIWA KIGOMA

KIGOMA, Septemba 4, 2026 — Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imemhukumu Nicholaus Komba Mahitana maarufu kama Abdallah Mahimbo baad...