Friday, January 03, 2025

WAZIRI NDEJEMBI AKUTANA NA WAMILIKI WA SHAMBA LA KWASHEMSHI LA KOROGWE

 










WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya kikao cha pamoja na Wamiliki wa Shamba la Sisal Estate “Kwashemshi” lililopo Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa muda mrefu baina ya wananchi wa eneo hilo na wamiliki hao.

Kikao hicho kimefanyika Januari 03, 2025  Ofisi za Makao Makuu ya Wizara zilozopo Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Netho Ndilito, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Mzava, Mkurugenzi wa Halmashauri ua Wilaya ya Korogwe Goodluck Mwangomango, Viongozi wa Sisal Estate wakiongozwa na Wakili Ndurumah Magembe na Mathew Kashindye pamoja na wajumbe wa Mejimenti na wataalamu wa wizara.

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...