Monday, January 22, 2007

Balozi Mahalu kizimbani

ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, amepandishwa kizimbani katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, kwa makosa sita ya uhujumu uchumi, wizi na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh2 bilioni.

Balozi Mahalu alitiwa mbaroni na maafisa wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (Takuru) pamoja na watu wengine wawili waliokuwa maofisa wa Ubalozi wa Tanzani nchini humo ambao nao wanaohusishwa na tuhuma hizo. Wengine ni Steward Migwano ambaye alikuwa Mtunza Fedha na Grace Martin ambaye alikuwa Afisa Utawala ubalozini hapo.

Watuhumiwa hao walifikishwa katika mahakama hiyo ya Kisutu asubuhi ya leo wakiwa kwenye gari la Takuru aina ya Toyota Landcruiser lenye namba za usajili T385 ALK na kusomewa mashtaka hayo yanayohusiana na upotevu wa Euro 2,065,827.60 wakati wakiwa maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Italia. Euro ni sawa na Sh1,692.74.

No comments:

RAIS DKT.MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON FUMBA, AANGALIA MAENDELEO YA UWANJA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi , leo Aprili 14, 2026, ameandika historia mpya baada ya kukagua ma...