Friday, July 11, 2008
Barabara ya Mandela
Bunge letu bwana

HAWA jamaa wa hili Bunge letu wa ajabu sana maamuzi yao pia ya ajabu ajabu hebu cheki uamuzi wao huu wa Tume ya Huduma za Bunge na Kamati ya Uongozi juu ya uchunguzi wa kuwapo kwa madai ya kumwagwa kwa unga kwenye ukumbi wa taasisi hiyo ambao sasa unamfunga mdomo Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge.
Chenge ambaye aliapa kupambana hadi hatua ya mwisho kusafisha jina lake kwa kile alichodai kuhusishwa na tuhuma za kumwagwa kwa unga huo kwenye Ukumbi wa Bunge, sasa hataweza kufanya lolote baada ya uamuzi uliotolewa jana kwamba, suala hilo limefikia ukomo na kwamba yeyote atakayezungumzia suala hilo kwa nia ya kudhalilisha Bunge au Spika atachukuliwa hatua.
Baada ya kuibuka kwa taarifa za kumwagwa kwa unga huo uliodhaniwa kwamba ni sumu ya kisasa, huku wengine wakihusisha na masuala ya kishirikina, Chenge alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kwamba, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alikuwa amemchafulia jina lake kwa kumhusisha na tukio hilo.
Chenge alisema kwamba, alikuwa na njia tatu za kupambana kudai haki yake, kwanza kulitumia Bunge; au kamati ya haki, wajibu na maadili ya Bunge au hata kwenda mahakamani kusafishwa jina lake. Soma Mwananchi kwa habari zaidi.
Chenge ambaye aliapa kupambana hadi hatua ya mwisho kusafisha jina lake kwa kile alichodai kuhusishwa na tuhuma za kumwagwa kwa unga huo kwenye Ukumbi wa Bunge, sasa hataweza kufanya lolote baada ya uamuzi uliotolewa jana kwamba, suala hilo limefikia ukomo na kwamba yeyote atakayezungumzia suala hilo kwa nia ya kudhalilisha Bunge au Spika atachukuliwa hatua.
Baada ya kuibuka kwa taarifa za kumwagwa kwa unga huo uliodhaniwa kwamba ni sumu ya kisasa, huku wengine wakihusisha na masuala ya kishirikina, Chenge alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kwamba, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alikuwa amemchafulia jina lake kwa kumhusisha na tukio hilo.
Chenge alisema kwamba, alikuwa na njia tatu za kupambana kudai haki yake, kwanza kulitumia Bunge; au kamati ya haki, wajibu na maadili ya Bunge au hata kwenda mahakamani kusafishwa jina lake. Soma Mwananchi kwa habari zaidi.
Thursday, July 10, 2008
Askofu Mokiwa mkali mno kwa mashoga
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Anglikana Nchini, Valentino Mokiwa, amesema anatamani kukalia kiti cha Kiongozi Mkuu wa Kanisa hilo duniani, Rowan William angalau kwa siku tatu ili aweze kutokomeza ushoga ndani ya kanisa hilo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mokiwa alieleza nia yake ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Kanisa hilo ulimwenguni, utakaofanyika katikati ya mwezi huu nchini Uingereza, huku nchi za Nigeria, Rwanda, Uganda na Kenya zikiwa zimetangaza kutoshiriki.
“Wengi walitazamia kiongozi wetu atoe kauli ya kuwatimua mashoga, alitakiwa kushika hatamu na kuonyesha njia…, kama ningepewa kiti chake angalau kwa siku tatu tu, ningewatimua mashoga na ninaamini tabia hii ingekoma, kwa sababu inakwenda kinyume na maandiko ya Matakatifu ya Mungu tunayemwamini,” alisema Mokiwa.
Alisema yeye ni miongoni mwa maaskofu wakuu 38 wa kanisa hilo duniani na kwamba, ingawa ndiye mdogo kuliko wote kiumri, alishamuandikia barua Askofu Mkuu wa Canterbury kumuomba awashughulikie wanaojihusisha na vitendo vya ushoga. Imeandikwa na Editha Majura.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mokiwa alieleza nia yake ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Kanisa hilo ulimwenguni, utakaofanyika katikati ya mwezi huu nchini Uingereza, huku nchi za Nigeria, Rwanda, Uganda na Kenya zikiwa zimetangaza kutoshiriki.
“Wengi walitazamia kiongozi wetu atoe kauli ya kuwatimua mashoga, alitakiwa kushika hatamu na kuonyesha njia…, kama ningepewa kiti chake angalau kwa siku tatu tu, ningewatimua mashoga na ninaamini tabia hii ingekoma, kwa sababu inakwenda kinyume na maandiko ya Matakatifu ya Mungu tunayemwamini,” alisema Mokiwa.
Alisema yeye ni miongoni mwa maaskofu wakuu 38 wa kanisa hilo duniani na kwamba, ingawa ndiye mdogo kuliko wote kiumri, alishamuandikia barua Askofu Mkuu wa Canterbury kumuomba awashughulikie wanaojihusisha na vitendo vya ushoga. Imeandikwa na Editha Majura.
Miss Tanzania wangia Kempu


Vimwana wa Miss Tanzania 2008 wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kuanza safari yao kuelekea bagamoyo kuanza kambi yao kabla ya mashindano hayo yanayotarajia kufanyika agosti 2 mshindi wa kwanza atapata gari na pamoja na shuilingi milioni nane na laki nane, wa pili atavuta milioni sita wakati wa tatu ataondoka na milioni tatu na laki nane, wa nne milioni mbili na laki saba na wa tano atakunywa milioni mbili na laki mbili.Asante Picha ya braza Michu.
Zitto alazwa
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akisumbuliwa na ugonjwa wa homa ya matumbo.
Akizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam hospitalini hapo jana, Msaidizi wa Mbunge huyo, Omary Ilyas, alisema Kabwe alilazwa tangu juzi usiku katika jengo la Mwaisela, wodi namba nane, chumba 312 baada kuugua ghafla, lakini sasa anaendelea vizuri kufutia huduma kutoka kwa madaktari wa hospitali hiyo.
“Alifikishwa hapa saa tatu usiku wa kuamkia jana. Tunadhani tatizo lake linatokana na uchovu wa safari madaktari wake wameshachukua vipimo vyote, tunasubiri ni majibu na anaweza kuruhusiwa kwani kwa sasa anaendelea vizuri,” alisema Ilyas na kuongeza:
“Mheshimiwa Mbunge amekuwa na ziara mfululizo, bila kupata mapumziko kwa kipindi kirefu, hivyo inawezekana ndizo ziliyomsababishia maumivu makali ya mwili kiasi cha kumlazimu alazwe hapa kwa ajili ya mapumziko na uchunguzi zaidi”.
Aliongeza kuwa baada ya kufikishwa hospitalini hapo alipokelewa na jopo la madaktari bingwa na baada ya kupatiwa huduma ya kwanza walichukuwa vipimo mbalimbali kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusu matatizo aliyonayo.
Hata hivyo baadaye jioni, alipozumgumza Mwananchi Ilyas alisema madaktari wamegundua kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa homa ya matumbo (typhoid), ambao umemsababishia homa kali na mwili kukosa nguvu.Imeandikwa na Jackson Odoyo na Saida Amini.
Wednesday, July 09, 2008
Miss Temeke
Subscribe to:
Posts (Atom)
MTUHUMIWA WA “KUFUTA MADENI” YA MIKOPO AKIRI KOSA, AHUKUMIWA KIGOMA
KIGOMA, Septemba 4, 2026 — Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imemhukumu Nicholaus Komba Mahitana maarufu kama Abdallah Mahimbo baad...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Nadhani mtakumbuka kibwagizo maarufu katika TV ambacho kinaimbwa perupe pepero perupe pepero hawa ni vijana wa Sisi Tambala waliokuwapo kati...
-
Mdau Julius Samwel hivi karibuni alikuwa huko Mwanza na hizi ndizo alizofanikiwa kutumegea, wadau hebu someni hicho kibao mniambie kuna nini...

