Katika hafla yenye utofauti, heshima na hamasa mpya kwa Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Novemba 14, 2025, amemuapisha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini, pamoja na wananchi waliojitokeza kushuhudia hatua hiyo muhimu katika uongozi wa nchi.
Dkt. Mwigulu, ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za juu serikalini, ametajwa kuwa miongoni mwa viongozi wenye rekodi ya utendaji, uthabiti wa uongozi na uwezo wa kusimamia mageuzi ya kiuchumi na kijamii. Uteuzi wake unaangaliwa kama mwanzo mpya wa msukumo wa kasi katika utekelezaji wa agenda za maendeleo zinazolenga kuinua maisha ya Watanzania.
Rais Dkt. Samia alisisitiza umuhimu wa uadilifu, uwajibikaji na kasi ya utendaji katika kuwatumikia wananchi, huku akimtaka Waziri Mkuu mpya kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya kimkakati, kuimarisha uchumi na kuhakikisha huduma za kijamii zinawafikia wananchi kwa ufanisi na usawa.
Wananchi na wadau mbalimbali nchini wamepokea tukio hilo kwa matumaini mapya, wakiona uteuzi huo kama chachu ya kuimarisha mwelekeo wa Taifa katika ujenzi wa uchumi shindani, Serikali shirikishi na maendeleo endelevu.

.jpeg)
.jpeg)



No comments:
Post a Comment