Tuesday, August 14, 2018

WAZIRI LUKUVI AFANYA ZIARA KATIKA ENEO LA SAFARI CITY

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akiwasili katika eneo la Mtradi wa Safari City jijini Arusha.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akiongozana na Meneja wa NHC mkoa wa Arusha, Ladislaus Bamanyisa na Afisa Mauzo na Masoko wa NHC, Neema Mapunda wakati akitembelea nyumba za mfano za Safari City jijini Arusha jana akiwa katika ziara hiyo Waziri Lukuvi  amelitaka Shirika  kuongeza juhudi za kuutangaza mradi pia kutumia ujenzi wa barabara ya East Afrika inayopita katika mradi wa safari city kama sehemu ya matangazo au kivutio cha mradi huo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mkoa wa Arusha alipotembelea mradi wa Safari City. 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akijadiliana jambo na Meneja wa NHC mkoa wa Arusha, Ladislaus Bamanyisa na Afisa Mauzo na Masoko wa NHC, Neema Mapunda wakati akitembelea nyumba za mfano za Safari City jijini Arusha jana.

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akiangalia michoro ya mradi wa Safari City akiongozana na Meneja wa NHC mkoa wa Arusha, Ladislaus Bamanyisa wakati akitembelea nyumba za mfano za Safari City jijini Arusha jana.


No comments: