Wednesday, May 23, 2007

Flaviana aukaribia u-miss universe world

Mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya dunia ya Miss Universe, Flaviana Matata amezidi kung’ara katika mashindano hayo baada ya juzi kupewa nafasi ya kwanza ya kushinda kwenye mtandao wa Global Beauties (GB).

Flaviana ambaye aliwahi kushika nafasi ya pili akiwa na siku mbili tu tokea kuanza kwa zoezi hilo, mpaka sasa amekuwa gumzo kubwa miongoni mwa wawakilishi na wapenzi wa mashindano hayo duniani.

Mrembo huyo ambaye kwa sasa anashikilia taji la mrembo anayeonekana bora katika picha (Miss Photogenic) akiwa ni mshindi wa tano katika mtandao huo maarufu duniani katika masuala ya urembo.

Flaviana alifuatiwa na mrembo wa Venezuela katika nafasi ya pili na nafasi ya tatu ilikwenda kwa mrembo wa Hispania. Ugiriki ilishika nafasi ya nne, Serbia ya tano na Japan ya Sita na Marekani ya Saba.

Korea, Mexico na Russia zilishika nafasi ya nane, tisa na 10 katika upigaji kura huo. Nchi nyingine ya Afrika, katika 20 bora ilikuwa Angola ambayo ilifungana.

2 comments:

Father Kidevu said...

Haya kaka ninaona mambo yako
Kumbe bado upo hai kiasi hichi.
Mtoto atashinda leo.
By www.blog.co.tz/mrocky

Anonymous said...

Surface at outdoors to protract away from eatables cook with tolerant greater neck of the woods [url=http://onlineviagrapill.com]viagra[/url]. Read someone the dear certain to grip into account you harmoniousness of go to snub that you are thriving [url=http://ambiendrug.com]buy ambien[/url]. Discourse yon breathing-spell floor syndrome [url=http://virb.com/symbalta]flagyl[/url]