Thursday, May 25, 2006

Watoto shuleni



Wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili katika Shule ya Msingi Twende Pamoja, iliyopo katika kijiji cha Mwamalili, Wilaya ya Shinyanga mjini, Tanzania wakigawiwa chakula cha mchana na wenzao, ikiwa ni katika mpango wa kupunguza utoro na kuongeza ubora wa elimu unaosimamiwa na Shirika la Kimataifa la Misaada la Oxfam, tangu kuanza kwa mpango huo mahudhurio ya watoto yameongezeka. (Picha na Yahya Charahani)Toa maoni yako.

5 comments:

boniphace said...

Mzee wa mshitu tupe taarifa zaidi kuhusu elimu ya hapo huko nyuma na sasa imeongezeka vipi na tazama na sababu zingine hasa makazi ya vijiji hivyo na watu wake isiwe shule inatumika kama sehemu ya kukimbia njaa hali inayoweza kuwafanya watoto hao kutokusoma kwa umakini na badala yake kuwaza muda wa maakuli tu.

Jeff Msangi said...

Yaani ina maana hawa Oxfam wameshindwa kabisa kutengeneza japo ka-karo ili watoto wagawiwe chakula kwenye mazingira bora zaidi?Hapo nje vumbi vipi?Au ni kwanini wazazi wasijitolee nguvu wakajenga wao karo?nikisema karo namaanisha sink.

Mija Shija Sayi said...

Jamani wana-shinyanga tumezidi bado tuko nyuma mno!! Vipi Charahani mwenzangu wewe ni Mwanza au Shinyanga?..hebu tufanyeni jamani tuuokoe mkoa wetu.

mzee wa mshitu said...

Makene umesema kweli kabisa watoto wa huku wamegeuza shule sehemu ya kukimbia njaa wazazi nasikia mitaa ya huko wanawalazimisha watoto kwenda shule wakijua watapata msosi kwa maana hiyo kiwango cha elimu bado kitaendelea kuwa cha chini hata wakifanya hivi sababu taarifa nilizo nazo kata nzima kilipo kijiji hicho ina shule moja tu ya sekondari.

Jeff unadhani kama wameshindwa kuandaa mazingira mazuri mpaka mfadhili akaja wataweza kweli kujenga karo, kwanza hiyo shule ina walimu tisa tu kwa madarasa yote.

Mija afadhali Shinyanga ipo mikoa hapa nchini hata shule za namna hii ni dili, mimi nimewahi kuishi Shinyanga lakini si mtu wa huko tunapaswa tupiganie maisha ya hawa vijana wetu kwani hali ni chafu.

Alex Mwalyoyo said...

NJAA HII HAISAHAULIKI!
Mh! Hii njaa ilikuwa kali sana, ilikuwa bila kugawa chakula kwa wanafunzi basi hakuna mahudhurio mazuri. Hali ilikuwa mbaya sana katika Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga. Tuombe Mungu baa hili lisirudie.
Karibuni kwangu 'http://jadili.blogspot.com'