Tuesday, April 10, 2012

HAIJAPATA KUTOKEA MAZIKO YA KANUMBA

Mmoja wa waombolezaji akipitishwa juu juu kwenye vichwa vya waombolezaji ili kupata huduma ya kwanza baada ya kuzirai, katikati anayetazama mbele ni Mussa Kisoky Mkurugenzi wa kampuni ya Sofia Production ya jijini Dar es salaam.
Rais wa Shirikisho la wasanii wa Filamu Saimon Mwakifwamba akizungumza katika msiba huo kutoa salamu zao za rambirambi kwa marehemu Steven Kanumba
Askari wa kike wakiweka sawa utaratibu wa waombolezaji kupita katika eneo hilo ili kukaa.
Ndugu wa karibu wakielekea sehemu waliyotengewa kukaa.
Mwigizaji Steven Jacob kushoto akizungumza jambo na mbunge wa Maswa Mashariki Mh. John Shibuda katikati.
Jeneza la mwili wa marehemu Kanumba likiwa limewekwa tayari kwa waombolezaji kutoa heshima zao za mwisho
Kundi maalum lililoandaliwa kwa nyimbo za maombolezo likiimba nyimbo za maombolezo katika katika msiba huo.
Mama wa Marehemu Steven Kanumba Flora Mtegoa akiwa katika hali ya majonzi mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akimfariji Mama Kanumba
Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi, Ridhiwan Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Idd Azzan na waombolezaji wengine wakiwa katika msiba huo.
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi akipiga sal;ute mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Steven Kanumba kama ishara ya kumkubali kwake na kutoa heshima kwa marehemu Steven Kanumba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Steven Kanumba ulioagwa leo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam huku viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, Wanasiasa, Wanamuziki Waigizaji na watu maarufu wamejitokeza kuuaga mwili wa mwigizaji huo aliyekuwa maarufu zaidi nchini Tanzania na nje ya nchi pia, Marehemu Steven Kanumba anazikwa mchana huu kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam

Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,jijini Dar es Salaam asubuhi hii. Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Steven Kanumba asubuhi hii kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.akifuatiwa na Mkewe,Pamoja na Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete (mwenye nguo nyeupe kulia). Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu akitoa heshima za mwisho.

Mmoja wa waombolezaji akisidiwa na wafanyakazi wa msalaba mwekundu mara baada ya kuzimia katika msiba huo mkubwa.
Picha zote hizi ni kwa hisani ya

http://www.fullshangweblog.com

Monday, March 19, 2012

Rais Jakaya Kikwete Amwapisha Meja Jenerali Samwel Ndomba Kuwa Mkuu Mpya wa JKT

Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi mkuu mpya wa JKT meja Jenerali Samwel Ndomba wakati wa hafla ya kumuapisha iliyofanyika leo asubuhi ikulu jijini Dar es Salaam.

Amiri Jeshi mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(Katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange(kushoto) na Mkuu mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo.Picha na Freddy Maro-IKULU

Dk Mwakyembe yuko fiti!!

Naibu Waziri wa Ujenzi Dk Harrison Mwakyembe akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam ofisini kwake kuhusiana na maendeleo ya Afya yake nakusema kwamba yeye sasa yuko fiti kiafya, na ameripoti ofisini rasmi leo hii alipoulizwa maswali kutoka kwa waandishi wa habari akasema mambo yote anaichia serikali kupitia tume maalumu iliyoundwa kufutilia suala la ugonjwa wake. (PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)

Dr Mwakyembe akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari mbalimbali leo ofisini kwake

Wednesday, March 07, 2012

CRDB Bank -Customer Information

Greetings.

Kindly note BOT has issued circular recently to commercial Banks, the circular requires clients to update particulars of their accounts.

The forms for updation of customers information can be found in CRDB Bank’s website under resources centre. The dully filled forms can be mailed in a scanned format to customer-hotline@crdbbank.com or send directly to respective branch before 14/03/2012.

I look foward to receiving maximum cooperation and timely filling of the forms.

NB; I have attached the Customer KYC Update Forms with this email and please you may share this information with other Tanzanians.

Regards,

Crispin S

RM-Tanzanite Account

President Kikwete presents Country Assesment Report to APRM team of experts


President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete presents the Tanzania Country Assessment Report to an APRM (Africa Peer Review Mechanism) Lead Panelist Barrister Mr. Akere Muna. during a function held at State House Gardens in Dar es Salaam, this morning. (photo by Freddy Maro).

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi(CCM) Nape Nnauye Akutana na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimfafanulia jambo Balozi Msaidizi wa Uingereza Hapa nchini, Susie Kitchens wakati wa mazungumzo yake na Mkugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (hayupo pichani) aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkaribisha Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (kushoto) aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Katikati ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (Wapili kushoto) baada ya mazungumzo yao leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens

Sunday, February 26, 2012

TABORA BOYS WAKUTANA MBALAMWEZI BEACH

Mwenyekiti wa Mkutano wa Wana Tabora Boys, Edwin Kidiffu wa kwanza kulia ambaye pia ni mwanasheria wa Ewura akimsikiliza kwa makini Makwinya aliyeinua mikono juu akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika ufukwe wa Mbalamwezi, wanaomsikiliza ni Bina Katikiro mwenye fulana ya bluu


Mzee wa Mshitu akiwapo kwenye mjadala uliokuwa ukiendelea kwa baadhi ya wana Tabora Boys Secondary School waliopata kusoma katika shule hiyo kongwe na yenye sifa tele nchini walipokutana jioni ya jana katika ufukwe wa Mbalamwezi jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine ilikuwa ni kukutana, kutafakari na kujadili way forward ya wana Tabora School hao.

Braza Kamtande Sikalwanda (Mchawi wa hesabu) aliyeipandisha chati mno Sekondari ya Tabora enzi hizo (katikati) akijadili jambo na Braza Kipeya wakati wa mkutano huo wa wana Tabora Boys uliofanyika jana katika Ufukwe wa Mabamwezi. Anayewashuhudia kulia ni Danny Lyimo.

Makwinya naye alikuwapo, huyu jamaa enzi hizo akiwa Tabora Boys alikuwa mkoba wa kutumainiwa wa timu ya shule na hasa pale timu ilipoweza kuitandika timu ngumu ya Uyui Sekondari mabao mawili kwa bila jambo lililizua balaa. Hapa jamaa anapiga maji ya mende.


Dokta Mzee Gombo ambaye ni Specialist wa Meno Muhimbili enzi hizo alikuwa PC wa PCB kwa lugha rahisi alikuwa kiranja wa darasa la wakali wa kombinesheni ya PCB akiwa na akina Charles Sebastian na Rahim Mzee, kwa mbali waweza kumuona Second Chief George, ambaye sasa ni daktari wa magonjwa sugu.

Palipo na picha, mara nyingi pana simulizi isiyoandikwa. Lakini kwa wazoefu wa maisha ya Tabora Boys, kila taswira huibua mlolongo wa kumbukumbu—za jasho, udugu, na nyakati zilizowatengeneza kuwa watu walivyo leo. Katika picha iliyopigwa hivi karibuni, Danny Lyimo anaonekana akishuhudia tukio lisilo la kawaida: Makwinya akisalimiana kwa hisia na Luwaga Kizoka—maarufu kama Nyigu. Nyuma yao, Renasco Mbilinyi anasimama kimya, lakini uso wake unaeleza mengi kuliko maneno.

Ni salamu ya kawaida, lakini pia ni ishara ya muda uliopita—wakati ambao ulikuwa mgumu lakini wenye fadhila za maisha. Salamu hiyo inavunja ukuta wa miaka, inafuta vumbi la kimya, na kuunganisha upya mioyo iliyounganishwa zamani na kiapo kisichoandikwa cha udugu wa Tabora Boys.

Danny Lyimo, kwa macho makini, hachungulii tu watu wawili wakisalimiana. Anaona nyuma ya pazia—miaka ya mafunzo ya kijeshi, zaezi la range, sindicate, sare za khaki, na nderemo za uwanjani. Anaona watoto waliogeuzwa wanaume. Anaona familia iliyozaliwa si kwa damu, bali kwa historia na kushirikiana katika kila hali.

Nyigu, kama alivyofahamika shuleni, hakuwa jina tu—alikuwa nembo ya msimamo. Makwinya, kwa salamu hiyo, hakumkumbatia mtu bali kumbukumbu nzima ya enzi zao. Na Renasco, japo nyuma ya pazia, anashuhudia ushahidi wa udugu unaovuka wakati, umbali na hadhi.

Tukio hili dogo lina ujumbe mkubwa: Urafiki wa kweli hauzeeki. Haubadilishwi na miongo wala majina ya vyeo. Huo ni urafiki uliopikwa kwa jua la Tabora, ukakomazwa na kwata, na kufungwa kwa heshima ya sare na ndoto za baadaye.

Kwa wengi, salamu hii ya kawaida ni picha tu. Lakini kwa familia ya Tabora Boys, ni waraka wa historia unaoandikwa upya—ushahidi wa kuwa nyakati hubadilika, lakini mioyo iliyounganishwa katika ujana huendelea kupigana kwa mdundo mmoja, hata miaka mingi baadaye.

Na timu ya Mzee wa Mshitu, kama kawaida, inaahidi kuwaletea picha na taarifa zaidi—kwa sababu kumbukumbu hizi si mali ya waliokuwepo tu, bali ni urithi wa wote walioguswa na utukufu wa Tabora Boys.

MTUHUMIWA WA “KUFUTA MADENI” YA MIKOPO AKIRI KOSA, AHUKUMIWA KIGOMA

KIGOMA, Septemba 4, 2026 — Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kigoma imemhukumu Nicholaus Komba Mahitana maarufu kama Abdallah Mahimbo baad...