Sunday, February 26, 2012

TABORA BOYS WAKUTANA MBALAMWEZI BEACH

Mwenyekiti wa Mkutano wa Wana Tabora Boys, Edwin Kidiffu wa kwanza kulia ambaye pia ni mwanasheria wa Ewura akimsikiliza kwa makini Makwinya aliyeinua mikono juu akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika ufukwe wa Mbalamwezi, wanaomsikiliza ni Bina Katikiro mwenye fulana ya bluu


Mzee wa Mshitu akiwapo kwenye mjadala uliokuwa ukiendelea kwa baadhi ya wana Tabora Boys Secondary School waliopata kusoma katika shule hiyo kongwe na yenye sifa tele nchini walipokutana jioni ya jana katika ufukwe wa Mbalamwezi jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine ilikuwa ni kukutana, kutafakari na kujadili way forward ya wana Tabora School hao.

Braza Kamtande Sikalwanda (Mchawi wa hesabu) aliyeipandisha chati mno Sekondari ya Tabora enzi hizo (katikati) akijadili jambo na Braza Kipeya wakati wa mkutano huo wa wana Tabora Boys uliofanyika jana katika Ufukwe wa Mabamwezi. Anayewashuhudia kulia ni Danny Lyimo.

Makwinya naye alikuwapo, huyu jamaa enzi hizo akiwa Tabora Boys alikuwa mkoba wa kutumainiwa wa timu ya shule na hasa pale timu ilipoweza kuitandika timu ngumu ya Uyui Sekondari mabao mawili kwa bila jambo lililizua balaa. Hapa jamaa anapiga maji ya mende.


Dokta Mzee Gombo ambaye ni Specialist wa Meno Muhimbili enzi hizo alikuwa PC wa PCB kwa lugha rahisi alikuwa kiranja wa darasa la wakali wa kombinesheni ya PCB akiwa na akina Charles Sebastian na Rahim Mzee, kwa mbali waweza kumuona Second Chief George, ambaye sasa ni daktari wa magonjwa sugu.

Danny Lyimo akishuhudia wakati Makwinya akisalimiana na Luwaga Kizoka (Nyigu) , nyuma yake anaonekana Renasco Mbilinyi. Taarifa na picha zaidi za matukio hayo zitaletwa kwenu na timu ya Mzee wa Mshitu.

5 comments:

Anonymous said...

Naam mzee wa Mshitu nimekusoma kaka... Safi sana hii... Next time when we meet we should come with a bang... Boyzia Always

Anonymous said...

Mzee wa Mshitu hiyo nimeiona! Wanafamilia ya Milambo Wanaume nayo Vp?

Anonymous said...

sawa sawa mmenikumbusha pande za orchard, tuko pamoja makamanda wangu

Anonymous said...

sawa kabisa inabidi tuitishe na siku ya walambo pia i hope wanakumbuka kwa mama white na kule ngoma sakas kwa wa-BIKS

Anonymous said...

Kwa Mama Joha pia usipasahau!