Saturday, May 03, 2025

MHE.MCHENGERWA ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHUMI LA ARUSHA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI,  Mhe. Mohamed Mchengerwa ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria  jukwaa la uchumi Arusha linalofanyika katika Ukumbi wa IACC Arusha.

Kongamano hili limejumuisha zaidi ya wadau 1000 kutoka maeneo mbalimbali duniani na kushirikisha mawaziri kadhaa wa sekta za tofauti.

Mwanamajumui wa Afrika Profesa Patrick Lumumba  pia amealikwa kuwa miongoni mwa watoa mada.

Jukwaa hilo limeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kupata ujuzi wa namna ya kutumia fursa za uchumi zilizopo mkoani Arusha.

No comments:

WMA YAFUNGA MTAMBO WA KISASA UNAOHAKIKI DIRA ZA MAJI DODOMA

Mtambo wa kisasa unaotumika kuhakiki dira za maji. Mtambo huu wa kidijitali umefungwa katika Jengo la Makao Makuu ya Wakala wa Vipimo (WMA),...