Saturday, May 03, 2025

MHE.MCHENGERWA ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHUMI LA ARUSHA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI,  Mhe. Mohamed Mchengerwa ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria  jukwaa la uchumi Arusha linalofanyika katika Ukumbi wa IACC Arusha.

Kongamano hili limejumuisha zaidi ya wadau 1000 kutoka maeneo mbalimbali duniani na kushirikisha mawaziri kadhaa wa sekta za tofauti.

Mwanamajumui wa Afrika Profesa Patrick Lumumba  pia amealikwa kuwa miongoni mwa watoa mada.

Jukwaa hilo limeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kupata ujuzi wa namna ya kutumia fursa za uchumi zilizopo mkoani Arusha.

No comments:

SERIKALI YATOA ZAIDI YA BILIONI 5.7 KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA ELIMU MKOANI KIGOMA

KIGOMA: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP), imetoa zaidi ya Shilin...