Saturday, May 03, 2025

MHE.MCHENGERWA ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHUMI LA ARUSHA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI,  Mhe. Mohamed Mchengerwa ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria  jukwaa la uchumi Arusha linalofanyika katika Ukumbi wa IACC Arusha.

Kongamano hili limejumuisha zaidi ya wadau 1000 kutoka maeneo mbalimbali duniani na kushirikisha mawaziri kadhaa wa sekta za tofauti.

Mwanamajumui wa Afrika Profesa Patrick Lumumba  pia amealikwa kuwa miongoni mwa watoa mada.

Jukwaa hilo limeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kupata ujuzi wa namna ya kutumia fursa za uchumi zilizopo mkoani Arusha.

No comments:

MMUYA: WANANCHI WANUFAIKE NA UWEKEZAJI WA NHC KUPITIA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amekagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maghala unaotekelezwa na S...