Monday, May 14, 2018

KATIBU MKUU WA WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI DOROTHY MWANYIKA AFUNGUA KIKAO CHA BARAZA KUU NHC


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa kinachofanyika leo jijini Dar es Salaam kinachojadili kwa mapana masuala ya utendaji kazi, maslahi ya wafanyakazi, utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka 10 wa Shirika na kujadili bajeti ya Shirika na utekelezaji wake. Kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Manyama Maagi na Kushoto kwake ni Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Mecktilda Mihayo na Wa kwanza Kushoto ni Naibu Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Adolf Kasegenya.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akishiriki wimbo wa pamoja wa wafanyakazi maarufu kama "Solidarity Forever"na Viongozi wa Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felix Manyama Maagi (wa pili kushoto) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, kushoto ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Adolph  Kasegenya na kulia ni Katibu wa Baraza, Mecktilda Mihayo wakazi wa kikao cha baraza hilo kinachofanyika kwa siku mbili makao makuu ya 
Shirika hilo Kambarage House.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akisindikizwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felix Manyama Maagi (katikati) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, kulia ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Adolph  Kasegenya baada ya ufunguzi wa kikao cha baraza hilo kinachofanyika kwa siku mbili makao makuu ya Shirika hilo Kambarage House.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Manyama Maagi akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa  huku Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika . Kulia kwake ni Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Mecktilda Mihayo na Kushoto ni Naibu Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, Adolf Kasegenya.


 Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akisindikizwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felix Manyama Maagi (katikati) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, kulia ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Adolph  Kasegenya baada ya ufunguzi wa kikao cha baraza hilo kinachofanyika kwa siku mbili makao makuu ya Shirika hilo Kambarage House.

 Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akisindikizwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felix Manyama Maagi (katikati) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, kulia ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Adolph  Kasegenya baada ya ufunguzi wa kikao cha baraza hilo kinachofanyika kwa siku mbili makao makuu ya Shirika hilo Kambarage House.
Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika na baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa
 


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dorothy Mwanyika akisindikizwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felix Manyama Maagi (katikati) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, baada ya ufunguzi wa kikao cha baraza hilo kinachofanyika kwa siku mbili makao makuu ya Shirika hilo Kambarage House.


HOTUBA YA KATIBU MKUU WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, DOROTHY MWANYIKA KWENYE UFUNGUZI WA KIKAO CHA BARAZA KUU LA WAFANYAKAZI LA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC), JIJINI DAR ES SALAAM TAREHE 14/05/2018.

Ndugu Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC na  Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Wafanyakazi,  Felix Manyama Maagi,

Ndugu Wakurugenzi wa Shirika,

Ndugu Wajumbe wa Baraza,

Ndugu Wageni Waalikwa,

Ndugu Wanahabari,

Mabibi na Mabwana.

Nianze kwa kueleza faraja yangu kwa mapokezi yenu mliyonipa na kuishukuru Menejimenti ya Shirika kwa kunipa heshima ya kuja kuwafungulia kikao hiki cha Baraza Kuu la Wafanyakazi. Nawashukuru kwasababu tukio hili la leo linanipa fursa ya kukutana na watendaji wakuu na wawakilishi wa wafanyakazi kutoka mikoa yote ya Shirika kwa mara ya kwanza tangu niteuliwe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara yetu. Hivyo, ni fursa kwangu kuweza kufikisha ujumbe kwa wafanyakazi na umma juu ya Shirika letu.

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, kwanza kabisa naomba nitumie fursa hii kuwapa pole wote mliosafiri safari ndefu ya kuja hapa Dar es Salaam. Tumshukuru Mungu kwa kuwawezesha kufika hapa salama salimini.

Pili, Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, nimeelezwa kwamba ajenda za kikao Baraza hili zimejielekeza katika masuala ya utendaji wa Shirika. Aidha, nimeelezwa kuwa kikao chenu kitapitia mizania ya hesabu za Shirika kwa mwaka wa fedha 2018/2019, pamoja na kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi mlizozipanga kuendana na Mpango Mkakati wenu. Naupongeza sana utaratibu huu maana unaleta mezani utekelezaji wa majukumu ya kazi na kuanisha changamoto mnazokumbana nazo kwa nia ya kuzipatia ufumbuzi sahihi kwa pamoja.

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, Sina haja ya kusisitiza umuhimu wa ajenda zote hizi zilizoko mbele yenu, kwani naamini wajumbe wote wa Baraza hili mnatambua umuhimu wake. Hivyo ni matarajio yangu kuwa ajenda hizi, ambazo zinagusa uhai na maendeleo ya Shirika letu, mtazijadili kwa kina ili hatimaye muweze kutoka na maazimio ya msingi yatakayoliwezesha Shirika hili kuongeza tija na kukidhi matarajiyo ya umma wa Watanzania ambayo kwa sasa yako juu sana kutokana na imani mliyowajengea.


Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, Baraza hili ni jukwaa muhimu sana mahala pa kazi kwani ni kiunganishi kati ya Menejimenti na Wafanyakazi. Ni matumaini yangu kuwa mtaendelea kushirikiana ili kuleta ufanisi kwa Mamlaka na Taifa kwa ujumla. Hata hivyo ikumbukwe kuwa Serikali inazingatia sana suala la taasisi zake kuwa na mabaraza ya Wafanyakazi kwani yalianzishwa kisheria kwa madhumuni ya kuishauri Serikali katika ngazi za idara, taasisi na Wizara kuhusu usimamizi wa kazi na rasilimali watu, utekelezaji wa majukumu, kulinda haki na wajibu wa waajiri na wafanyakazi, kutoa ushauri kuhusu kujenga hali bora za kazi, maslahi ya Wafanyakazi na kusimamia haki na ustawi katika sehemu za kazi. Wajibu wa mabaraza haya kama vyombo vya ushauri na usimamizi ni kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao, pia wanazingatia maadili ya utumishi wao ili kuleta matokeo ya utendaji wa kazi yenye tija, staha na upendo.

Kadhalika, niwapongeze kwa kutengeneza na kisha kuufanyia mapitio Mpango Mkakati wa miaka kumi ambao mkiufanyia kazi na kuutekeleza kwa wakati mtaleta mabadiliko makubwa katika sekta ya nyumba hapa nchini. Nimesoma Mpango Mkakati huo kwa makini na kuyapitia malengo yote sita mliyojiwekea.

Nataka niwaambie kuwa malengo haya siyo mepesi, ni mazito na yanahitaji uwajibikaji wa hali ya juu ili kuweza kuyatekeleza kwa ufanisi la sivyo yatabaki kwenye makaratasi. Hivyo, nitoe rai kwenu kuwa muweke mbele maslahi ya Shirika na ushirikiano mkubwa ili muyafikie malengo yenu. Wakati nikiwapongeza kwa kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutekeleza Mpango Mkakati huu wa miaka kumi (2015/16-2024/25), ni vema mkajua kuwa Serikali imewapa dhamana kubwa ya kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya nyumba. Shirika lina changamoto ya kuhakikisha kuwa linakuwa na uwezo wa kifedha ili kuweza kutekeleza mikakati ya ujenzi wa nyumba hizi hasa nyumba za gharama nafuu. Niseme tu kuwa Wizara inaungana nanyi katika kuhahakikisha kuwa yale yote ambayo yanahitaji msukumo wa Wizara yanatekelezwa ili kuweza kufikia malengo mliyojiwekea kwa wakati.

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, Nipende kuwakumbusha kwamba Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kwa dhati, katika ujenzi wa uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu. Lengo kuu la Mpango huo ni kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati inayoongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025. Ni dhahiri, Shirika la Nyumba mtachochea azma hii ya viwanda kwa kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba na tija katika ujenzi.

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, kupitia hotuba yangu, napenda kuwahamasisha muendeleze ushirikiano na mabenki kutoa elimu ya mikopo ya nyumba ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kutumia fursa zilizopo za mikopo ya benki kununua nyumba zinazojengwa na Shirika. Itakuwa fahari kubwa kwa mwananchi kumiliki majengo ya ofisi, biashara na makazi katikati ya miji na Halmashauri zetu zinazojengwa na NHC.

Ndugu Mwenyekiti na Wajumbe, sitaki kuwachosha hata kabla hamjaanza kazi nzito iliyoko mbele yenu. Hivyo, naomba niishie hapa kwa kuishukuru tena Menejimenti kwa kunialika kuja kufungua kikao chenu hii leo. Aidha, naomba nimalizie kwa kuwatakia wajumbe wote safari njema mtakaporejea majumbani na sehemu zenu za kazi.

Baada ya kusema haya sasa napenda kutamka kuwa kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi kwa mwaka 2018, kimefunguliwa rasmi.  Asanteni sana kwa kunisikiliza.

No comments: