Monday, October 31, 2011

NHC yatiliana saini ya makubaliano ya mikopo ya nyumba na benki saba za hapa nchini

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba nchini, Nehemiah Mchechu akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya kutiliana saini ya makubaliano baina ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Mabenki ili kuwezesha kutoa mikopo ya Nyumba kwa wananchi hapa nchini. Hafla hii imefanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Nyumba Tanzania, Injinia Kesogukewele Msita akihutubia katika hafla hiyo.
Waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka akihutubia wakati wa hafla ya kutiliana saini ya makubaliano baina ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Mabenki ili kuwezesha kutoa mikopo ya Nyumba kwa wananchi hapa nchini. Hafla hii imefanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba Tanzania,Nehemiah Mchechu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB,Mark Wiessing wakitiliana saini ya makubaliano kuwezesha kutoa mikopo ya Nyumba kwa wananchi hapa nchini .Waliosimama wakishuhudia tukio hilo ni Waziri wa Ardhi, Profesa Anna Tibaijuka na Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la Nyumba Tanzania,Eng Kesogukewele Msita. Hafla hii imefanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Lawrence Mafuru akisoma hotuba yake fupi kwa niaba ya Mabenki ya hapa nchini wakati wa hafla ya kutiliana saini ya makubaliano baina ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Mabenki ili kuwezesha kutoa mikopo ya Nyumba kwa wananchi hapa nchini .hafla hii imefanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro,jijini Dar es Salaam.

No comments: