Saturday, January 26, 2019

NHC SINGIDA WAFANYA MATEMBEZI NA KISHA KUPANDA MITI ENEO LA UNYAKUMI

 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba Mkoa wa Singida leo wametekeleza wito wa kufanya matembezi uliotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Dk. Maulidi Banyani, pichani Wafanyakazi hao wa NHC Singida wakiendelea na zoezi la viungo baada ya 5km. Baada ya hapo walipanda miti katika eneo la Unyakumi.

 Mwanakijiji akishiriki kupanda miti kwenye eneo la Nyumba za gharama nafuu Unyakumi mkoani Singida leo asubuhi.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya akizindua  mradi wa kupanda miti 300 kwenye eneo la Nyumba za gharama nafuu Unyakumi mkoani Singida leo asubuhi, mradi  uliofadhiliwa na ant desert  environmental care na TFS
Wafanyakazi wa Singida wakielekea kwenye eneo la kuzindua kampeni ya kupanda miti 300 unyakumi baada ya mazoezi ya kutembea na viungo.

 Wafanyakazi wa Singida wakifanya mazoezi ya viungo baada ya kutembea 5 km.
 Wafanyakazi wa Singida wakiwa wanatoka Singidani complex ofisi inapohamia.
NHC Singida wakiendelea na mazoezi ya 5 km.

No comments: