Wednesday, July 27, 2011

Safari ya Mwisho ya Marehemu Danny Mwakiteleko


Gari la Mhariri wa gazeti la Rai na Naibu Mhariri Mtendaji wa New Habari, Danny Mwakiteleko, Danny alipata ajali Jumatano Julai 20, 2011 eneo la Tabata (ToT) na kukimbizwa katika Hospitali ya Amana, Ilala na baadaye Muhimbili.Katika ajali hiyo gari alilokuwa akiendesha Danny liligongwa na lori lenye trela, ambalo lilitoweka bila kujulik...ana saa nne usiku. Mwakiteleko alikuwa akitokea kazini Sinza ambako alifanya kazi hadi saa tatu usiku.—

Mwili wa Marehemu Danny Mwakiteleko ukihifadhiwa kaburini tayari kwa safari ya mwisho ya marehemu.


Misa ya kumwombea Marehehemu Danny Mwakiteleko ilifanyika katika Kanisa la KKKT Usharika wa Ndala. Na baade maziko kufanyika katika makaburi ya Masebe 1 kijijini Ndala, Kata ya Kandete, Tarafa ya Busokelo Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Danny alifariki Julai 23 kwa ajali ya gari na kuzikwa leo Julai 26, 2011.Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-Amen.


Watoto wa Marehemu Danny Mwakiteleko Vanesa kulia na Caroline kushoto pamoja na mama yao anayeonekana kufarijiwa wakionekana wenye simanzi kubwa katika mazishi ya mpendwa baba yao.
Kwa
Habari zaidi waweza kubonya hapaUpate tukio hilo kwa kina.

No comments: