KAULI ni kitu muhimu sana katika maisha ya binadamu yeyote awaye. Kauli yaweza kuchonganisha. Inaweza pia kufurahisha, kutoa matumaini, kuleta balaa wakati mwingine na hata kuleta madhara makubwa.
Kauli ndizo huweza kumtambulisha mtu na kutambua yukoje mbele ya wenzake. Huweza kuwafanya watu wengine watambue ni kiasi gani mtu wanayezungumza naye kaiva au kukomaa au vinginevyo.
Kwa jumla, kauli humchonganisha au kumkutanisha mtu na watu wengine. Kisiasa, kauli hujenga mtaji kwa mwanasiasa kukubalika na hasa kama anajua namna ya kuzipangilia hoja kimantiki, lakini hasa zikiwa zenye kubeba ukweli na uhalisia wa mambo.
Kwa kawaida, imezoeleka kuwa kauli nyingi zinazotoka midomoni mwa wanasiasa kuwa ni za uongo, huchukuliwa hivyo kwa sababu mara nyingi hutolewa ili kutumika kama chambo cha kuwavuta wananchi kuwachagua na kisha wakishawachagua wanawasahau. Lakini, si kweli wakati mwingine kuna ukweli fulani.Soma kwa urefu zaidi hapa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment