Thursday, March 28, 2019

NHC YAKABIDHIWA ENEO LA VINGUNGUTI KWA AJILI YA KUANZA UJENZI WA MACHINJIO YA KISASA

 Hili ndilo jengo la machinjio la sasa ambalo linatumia kuchinjia mifugo takribani 500 kwa siku wakati lilijengwa kwa ajili ya kuchinjia mifugo 25 tu eneo la Vingunguti Dar es Salaam. Eneo hili limekabidhiwa kwa Shirika la Nyumba la Taifa kama Mkandarasi kwa ajili ya kuliendeleza.
 Eneo la nyuma ya machinjio hayo kama linavyoonekana kwa sasa.
 Viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala na wa Machinjio wakilitembelea eneo hilo linalotarajiwa kujengwa machinjio ya kisasa.
 Viongozi wakishuhudia miundombinu ya upitishaji maji taka na masalia ya mifugo katika eneo la sasa la machinjio hayo,
 Msanifu wa Majengo kutoka Kampuni ya Cons Africa Limited, Joseph Mandwa akionyesha mchoro wa jengo jipya la machinjio litakavyokuwa.
 Viongozi hao wakiangalia kwa pamoja wakiangalia kwa pamoja mchoro huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Ubunifu, Margareth Ezekiel akimkabidhi Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto mchoro wenye ramani ya machinjio hayo