Friday, June 09, 2006

Wamjua kijana mwenye fikra za kiuanamapinduzi

KILA kukicha teknolojia ya habari na mawasiliano inazidi kujipenyeza ndani ya jamii yetu na kwa hakika kuzidi kukineemesha kijiji chetu kilichokuwa na kaya chache sana, nyingi zikiwa mbalimbali mno. Lakini tofauti na mwaka jana na mwaka ulee sasa kijiji chetu kimesheheni miji mingine sasa ni mighorofa mikubwa jana katika pitapita yangu nimebahatika kupita katika kaya ya ndugu yangu wanamwita Steve Biko ni kijana machachari sana huyu katika masuala ya kuutetea uafrika na utanzania kwa ujumla, fikra zake ni za kiuanamapinduzi. Waweza bonya hapana kutazama nini alichoweka maana kama ujuavyo fikra za kiuanamapinduzi ni uanamapinduzi kweli!

No comments: