* Kamati ya Bunge Yasema ina matumaini Makubwa na Hatua iliyofikiwa, Wapongeza Serikali kutoa fedha
* Ujenzi Wafikia Asilimia 92.8
📍 Dodoma
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameiambia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwamba, ifikapo Mei 15, 2025, Huduma zote za Wizara Makao Makuu, zitaanza kutolewa katika Jengo Jipya la Wizara Mji wa Serikali- Mtumba baada ya michakato yote kukamilishwa.
Amesema hayo leo Machi 20, 2025, wakati wa ziara ya Kamati hiyo ilipotembelea kukagua maendeleo ya mradi huo ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 92.8, huku kazi chache zilizobaki zikihusisha ukamilishaji wa masuala ya mifumo ya TEHAMA, zimamoto, rangi na samani za ndani ambapo tayari Wizara imekwisha kutangaza zabuni ya samani hizo.
‘’Mhe. Mwenyekiti, kukamilika kwa jengo hili kutaiwezesha Wizara kuwahudumia watanzania na wageni kutokea eneo moja na hivyo kutoa huduma kwa urahisi kuliko ilivyo sasa ambapo baadhi ya watumishi wako kwenye maeneo mengine ikiwemo katika eneo la ilipo Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na hapa Mtumba,’’ amesema Mhe. Mavunde.
Ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa kwa kuweka nguvu ili kukamilisha mradi wa Mji wa Serikali na kuweza kutoa kiasi cha shilingi bilioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa mji huo na kueleza kuwa, uwepo wa mji huo utasaidia kurahisisha utoaji huduma kwa Serikali na kuongeza kwamba, umeongeza mwonekano mzuri wa mji wa Dodoma huku akitolea mfano wa Nchi ya Malaysia kuwa na mfumo kama Mtumba.
Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. David Mathayo amesema kwamba Kamati hiyo ina matumiani makubwa kutokana na hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa jengo hilo na hivyo kutoa pongezi kwa Serikali kwa kutoa fedha kukamilisha majengo yaliyopo katika mji huo na kusema kwamba uwepo wa Wizara zote katika mji huo utarahisisha utoaji huduma kwa wawekezaji na watanzania kama ilivyo kwa nchi ya Brazil.
Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Mathayo ameumwagia sifa uongozi wa Wizara ya Madini kutokana na namna wanavyosimamia shughuli za Sekta ya Madini na kueleza kuwa, kitendo hicho kinatoa ahueni kwa kamati hiyo ambayo inasimamia Wizara za Madini na Nishati.
‘’Tunawafahamu namna mnavyochapa kazi, kamati yetu tuna furahi tuna viongozi walionyooka, ni viongozi, wazoefu na wachapakazi. Hatuna shaka kama kamati tunafurahi kwasaabu mnaisimamia wizara vizuri,’’ amesema Dkt. Mathayo.
Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Madini, Festus Mbwilo akisoma taarifa ya maendeleo ya mradi, ameieleza kamati kuwa Wizara imeendelea kusimamia kwa karibuni utekelezaji wa mradi huo ulioanzamwaka 2021 ili ukamilike kwa wakati ikiwemo kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza
Mkandarasi wa jengo la Wizara ya Madini ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na linajengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 22.8 na Mshauri Elekezi ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA