Friday, September 26, 2025

WANABLOGU SASA NI SEHEMU YA FAMILIA YA HABARI NCHINI

 







Mwandishi Wetu

Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) umeingia rasmi kwenye familia kubwa ya vyombo vya habari baada ya kukabidhiwa hati za uanachama katika Mkutano Mkuu wa 27 wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), uliofanyika Septemba 25, 2025 jijini Dar es Salaam. TBN ilikuwa miongoni mwa wanachama wapya wanane (8) waliopokelewa rasmi na Baraza.

Mwenyekiti wa TBN, Ndugu Beda Msimbe, alisema hatua hiyo ni mwanzo mpya kwa wanablogu nchini kwani inaleta heshima, uhalali na ulinzi wa kitaaluma.
“Uanachama huu unatoa uhalali wa kutambulika mbele ya jamii, Serikali na wadau wengine. Sasa wanablogu tumetambulika kama chanzo cha habari kinachowajibika na tunashirikiana na vyombo vingine vya habari katika kulinda maadili ya taaluma,” alisema Msimbe.

Aliongeza kuwa wanachama wa TBN sasa wananufaika na mfumo wa ulinzi wa Baraza, hususan katika usuluhishi wa malalamiko, jambo linalowalinda kisheria na kiuchumi dhidi ya vitisho vinavyoweza kuathiri maisha na kazi zao.

Katibu Mtendaji wa MCT, Bw. Ernest Sungura, alisisitiza mshikamano na mshikikiano wa wanachama, akibainisha kuwa kauli mbiu ya mkutano, “Uhai wa Wanachama ni Nguvu na Usalama wa Taaluma ya Habari”, inapaswa kuongoza kila chombo cha habari.
“Uhai wa Baraza upo mikononi mwa wanachama. Ni wajibu wetu kushiriki kikamilifu na kulipa ada ili taasisi hii iendelee kuimarika,” alisema.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Ndugu Yusuf Khamis Yusuf, alikumbusha kuwa kwa miaka 30 MCT imeendelea kujipambanua kama ngao ya uhuru na maadili ya habari nchini.

Akifungua mkutano huo, Rais Mstaafu wa Nne wa Baraza, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo, aliweka msisitizo mkubwa kwa wanahabari kusimama na ukweli bila kuyumba.
“Kusimama kwenye haki ni kugumu kuliko kujipendekeza. Ni njia yenye gharama, lakini ndiyo njia ya baraka na inayompendeza Mungu,” alisema huku akiwahimiza wanahabari kuendelea kuwa nguzo ya ukweli kwa jamii.

Katika tukio hilo pia, Jaji Mihayo alizindua rasmi Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT 2025) zitakazoendeshwa kwa mfumo wa kidijitali, pamoja na kuzindua tovuti mpya ya MCT, hatua inayothibitisha dhamira ya kuimarisha weledi na udugu ndani ya tasnia ya habari.

Kwa kupokelewa kwake MCT, TBN sasa si tu sauti ya wanablogu bali pia sehemu ya familia pana ya wanahabari nchini, ikionyesha mshikamano na mshikikiano wa kweli kwa ajili ya kulinda taaluma, kuendeleza uhuru wa habari na kudumisha mshikikiano wa vyombo vya habari Tanzania.


NGORONGORO YANADI FURSA ZA UTALII NA UWEKEZAJI ULAYA



Naibu Kamishna wa Uhifadhi, Huduma za Shirika Ngorongoro, Bw. Aidan Makalla (kulia), akiwa ameambatana na Abdiel Laizer, Afisa Utalii Mkuu Msaidizi, amekutana na mawakala mbalimbali wa utalii kunadi fursa za utalii na uwekezaji zilizopo Ngorongoro katika maonesho ya “My Tanzania Roadshow 2025 Europe”.

Maonesho hayo yanafanyika kuanzia Septemba 22 hadi 27, 2025 katika miji ya Stuttgart – Ujerumani, Salzburg – Austria, Ljubljana – Slovenia na Milan – Italia.

Tukio hilo linaratibiwa na Kampuni ya KILIFAIR na ni jukwaa la kipekee la kutangaza vivutio vya utalii, kuibua fursa mpya za uwekezaji na kuitangaza Tanzania kama kitovu cha utalii katika soko la Ulaya.

Ngorongoro, ikiwa ni moja ya hazina kubwa za malikale na urithi wa dunia, imeendelea kuwa kivutio cha pekee kinachochangia kwa kiasi kikubwa mapato ya taifa kupitia sekta ya utalii.

 Kwa kushiriki maonesho haya, Shirika la Hifadhi la Ngorongoro linaimarisha nafasi yake kimataifa kwa kuwavutia wawekezaji na kuendeleza mikakati ya kuongeza idadi ya watalii kutoka bara la Ulaya.

MAJALIWA AONGOZA MAZISHI YA ABBAS MWINYI








WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Septemba 26, 2025 ameshiriki katika maziko ya Abbas Ali Mwinyi ambaye ni kaka wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi yaliyofanyika Mangapwani, Zanzibar

TUME YA UTUMISHI WA UMMA KUANZA MKUTANO WA KWANZA WA 2025/26 JIJINI DODOMA

Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. John Chagama, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Septemba 26, 2025 jijini Dodoma, kuelekea Mkutano wa Kwanza wa Tume unaotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 29 Septemba hadi 17 Oktoba 2025 jijini Dodoma.


Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, John Chagama, amesema Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Utumishi wa Umma kwa mwaka wa fedha 2025/2026, unatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 29 Septemba hadi 17 Oktoba 2025 jijini Dodoma, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) eneo la Njedengwa.

Mbisso ametoa taarifa hiyo leo Septemba 26, 2025 jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema mkutano huo utakuwa ni fursa muhimu kwa Tume kupokea, kujadili na kutoa maamuzi juu ya rufaa na malalamiko mbalimbali yaliowasilishwa na watumishi wa umma ambao hawakuridhika na maamuzi ya waajiri wao, mamlaka za ajira na mamlaka za nidhamu.

“Tume ina wajibu wa kisheria kupokea hoja hizo chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma (Sura ya 298, marejeo ya 2023) pamoja na Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2022,”

“Tume ya utumishi wa umma imepanga kujadili na kutoa uamuzi wa rufaa na malalamiko mbalimbali zaidi ya mia moja yaliyowasilishwa na watumishi wa umma ambao hawakuridhika na uamuzi uliotolewa na waajiri, mamlaka za ajira na mamlaka zao za nidhamu,” amesema Mbisso

Chagama pia ameongeza kuwa katika mkutano huo, warufani au warufaniwa walioomba watapewa nafasi kupiga hoja zao mbele ya Tume, kutoa ufafanuzi wa ziada kuhusu rufaa zao, kama vile inavyowekwa wazi kwenye Kanuni ya 62(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma. 

Aidha, taarifa kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Tume kwa robo ya tatu na robo ya nne ya mwaka wa fedha 2024/2025 zitawekwa mbele ya wajumbe wa mkutano kwa majadiliano na utoaji wa mwelekeo.

Akizungumza juu ya umuhimu wa mkutano huo, Mbisso amesisitiza kwamba ni sehemu ya uwajibikaji wa Tume kuhakikisha utendaji kazi wa utumishi wa umma unafuatana na sheria, kanuni, taratibu na miongozo inayoweka haki na uwazi kwa watumishi wote. 

Katika hafla nyingine, amefungua kikao kazi cha ndani cha Tume ambapo aliagiza mapitio ya miongozo ya ndani, akisisitiza kuwa Tume lazima iendelee kujiboresha ili kuendana na mahitaji ya wakati na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma.

MAKAMU WA RAIS AHUTUBIA KIKAO CHA 80 CHA BARAZA KUU LA UMOJA WA TAIFA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Thabit Kombo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Zanzibar Kazi na Uwekezaji Mhe. Shariff Ali Shariff katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Mabalozi wa Tanzania mara baada ya kuhutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Thabit Kombo wakati akiondoka katika Jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani mara baada ya kuhutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania inalaani kuibuka upya kwa ukiukwaji wa sheria za kimataifa na kupelekea matumizi ya nguvu kama njia ya kutatua migogoro hali inayopelekea ukatili uliokithiri kwa binadamu hususani watoto, wanawake, wazee pamoja na wagonjwa katika maeneo ya migogoro.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akihutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani. Amesema uwepo wa mitazamo ya kibeberu, ikiwa ni pamoja na ile ya kuichukulia Afrika kuwa sehemu ya uchukuaji rasilimali na uporaji wa ardhi, pamoja na uwepo wa makampuni ya kimataifa kuendelea kufanikiwa kutokana na unyonyaji wa mali asili za Afrika, huku wakisababisha au kuunga mkono migogoro inapaswa kumalizika sasa.
Makamu wa Rais amesema Tanzania inauchukulia msimamo wa upande mmoja na matumizi mabaya ya nguvu za kijeshi, pamoja na kushindwa kwa jumuiya ya kimataifa na mataifa yenye nguvu duniani katika kukomesha umwagaji damu na vita vya hatari vinavyoendelea katika maeneo mengi duniani, kuwa ni jambo lisilokubalika.
Pia ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutambua kuwa ongezeko la matumizi ya fedha katika masuala ya kijeshi ikiwemo utafiti na utengenezaji wa silaha ni jambo la kusikitisha na ni kinyume cha maadili. Amesema hali hiyo inazuia jitihada za kutafuta amani duniani, na inachukua kiasi kikubwa cha rasilimali ambazo zingeweza kutumika kuendeleza maendeleo endelevu na ustawi kwa wanadamu wote.
Makamu wa Rais amesema dunia inapaswa kuendelea kutafuta amani bila kuchoka kwani ndio sharti la maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amepongeza juhudi za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, viongozi wa dunia, na mashirika ambayo yanashiriki kikamilifu katika upatanishi na utatuzi wa migogoro katika nchi na maeneo kama vile Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudan, Urusi, Ukraine, na Mashariki ya Kati. 
 Ametoa wito wa ushirikishwaji kamili wa wanawake katika kutafuta amani hususani katika kipindi hiki inaposherehekewa miaka 30 tangu azimio la Beijing na maendeleo yaliyopatikana katika kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.
Amesema Rais wa kwanza mwanamke wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ameonyesha njia katika kueleza sera na vitendo vinavyoimarisha nafasi ya mwanamke katika sekta zote za jamii. Amesema kikanda na kimataifa, amekuwa mtetezi wa amani, haki, usalama na matumizi ya nishati safi.
Amesema Tanzania kama mwanachama wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, pia nafasi iliyotumikia kama Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa Ulinzi na Usalama Jumuiya ya SADC ilichangia kikamilifu katika mipango ya amani na kuunga mkono hatua za kuzuia na kutatua migogoro.
Tanzania imetangaza kugombea kiti kisicho cha kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa muhula wa 2029-2030, ili kuthibitisha dhamira iliyonayo ya amani na usalama duniani.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema, Tanzania inasisitiza msimamo wa Afrika wa kurekebisha uwakilishi mdogo wa bara hilo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kutoa wito wa kupitishwa kwa angalau viti viwili vya kudumu vya Afrika vyenye nguvu ya kura ya turufu.
Amesema Tanzania inaungana na nchi nyingine katika kudai mageuzi ya haraka na ya kina ya mfumo wa fedha wa kimataifa. Ametoa wito wa kuongeza ufadhili wa masharti nafuu wa muda mrefu, kurekebisha mifumo huru ya ukadiriaji wa mikopo, na kufikiria upya tathmini ya uhimilivu wa deni, ili kupatikana mtaji wa uwekezaji katika miundombinu, elimu, afya na kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza nia ya kuongezeka kwa sauti na uwakilishi wa Afrika katika miundo ya utawala ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Dunia ambayo haijafanyiwa kazi kwa muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema Tanzania imejitolea na imepiga hatua katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s 2030) ikifikisha asilimia 60. Amesema kwa lengo namba 3, Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 750 kwa kila vizazi hai 1000 mwaka 2000 hadi 104 mwaka 2022. Kwa lengo namba 6, upatikanaji wa maji safi na salama uliongezeka katika maeneo ya vijijini na mijini kutoka asilimia 32 na 55 mwaka 2000 hadi asilimia 79.9 na 94 mwaka 2024. Kwa nishati safi ya bei nafuu ambayo ni lengo namba 7, Tanzania imefanikiwa kuunganisha nishati ya umeme kwa vijiji 8,587 mwaka (2000) hadi 12,318 mwaka 2024 ambapo ni vijiji 15 pekee vilivyobaki bila umeme.
Makamu wa Rais amehimiza jumuiya ya kimataifa kuimarisha mwitikio wa pamoja wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Ametoa wito wa kutumia vyema fursa ya Mkutano wa wa COP30 nchini Brazil kuhakikisha ahadi zinatekelezwa ikiwemo uchangiaji wa Mfuko wa Hasara na Maafa kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund) pamoja na kuongezwa kwa ufadhili wa masharti nafuu wa muda mrefu, uhamishaji wa teknolojia, na masharti ya kibiashara yanayozingatia haki ili kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa mataifa na kutafuta ushirikiano wa manufaa kwa pande zote katika matumizi ya rasilimali.

ECOBANK TANZANIA YAZINDUA TOLEO JIPYA LA ‘ELLEVATE’ KWA KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu akizungumza na Wanawake Wajasiriamali wadogo, wakati na wakubwa wakati wa kufungua semina ya mpango maalum ujulikanao kama ‘Ellevate by Ecobank’ iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Ecobank Tanzania, Joyce Ndyetabura akizungumza kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo kwa wanawake pamoja na wajasiriamali waliofika kwenye semina ya mpango maalum ujulikanao kama ‘Ellevate by Ecobank’ iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wanawake wajasiriamali pamoja na wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu alipokuwa anafungua semina ya mpango maalum ujulikanao kama ‘Ellevate by Ecobank’


Mdahalo uliojumuhisha wanawake wajasiriamali wadogo, wakati na wakubwa ukiendelea wakati wa semina ya ya mpango maalum ujulikanao kama ‘Ellevate by Ecobank’ 





 Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ecobank Tanzania pamoja na Wanawake Wajasiriamali mara baada ya kufungua semina ya mpango maalum ujulikanao kama ‘Ellevate by Ecobank’.
Ecobank Tanzania imezindua rasmi toleo lililoboreshwa la mpango wake wa "Ellevate by Ecobank", likiwa na lengo la kuharakisha ujumuishaji wa kifedha na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake wajasiriamali.
Awali, Ellevate ilianzishwa kusaidia biashara ndogo na za kati (SMEs) zinazoongozwa au kumilikiwa na wanawake. Hata hivyo, mpango huu sasa umeboreshwa na kupanuliwa ili kuwafikia wanawake katika sekta zote za biashara kuanzia makampuni makubwa, SMEs hadi wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Dkt. Charles Asiedu, alisema mpango huu umekuwa na mchango mkubwa kwa wafanyabiashara wanawake nchini.
“Wafanyabiashara wanawake wa Tanzania tayari wameshuhudia manufaa ya ‘Ellevate by Ecobank’. Tangu kuanzishwa kwake, tumewasaidia zaidi ya wanawake wajasiriamali 300. Toleo hili jipya linaimarisha dhamira yetu ya kuwa benki ya chaguo kwa wanawake wajasiriamali na kuendeleza nafasi yetu katika kusukuma mbele ujumuishaji wa kifedha barani Afrika,” alisema Dkt. Asiedu.
Aliongeza kuwa kupitia Ellevate, wanawake wa Afrika watapata huduma za kifedha za viwango vya kimataifa, zinazowawezesha kuongeza ukuaji wa biashara zao, kupata faida endelevu na kujiimarisha kwa muda mrefu.
Pia amesema miongoni mwa faida zinazotolewa kupitia mpango huu ni pamoja na mikopo isiyo na dhamana hadi kufikia Dola za Kimarekani 50,000, kupunguzwa kwa vikwazo vya kuingia kwenye mpango kwa historia ya miaka miwili ya biashara pekee badala ya mitatu, pamoja na masharti nafuu ya dhamana na viwango vya riba vinavyoshindana.
"Wanawake wajasiriamali watanufaika na fursa za kupanua masoko kupitia jukwaa la MyTradeHub linalowaunganisha na wateja wapya barani Afrika, pamoja na mafunzo ya kukuza uwezo wa biashara na uongozi, na upatikanaji wa huduma za bima, usimamizi wa mali na ulinzi wa mishahara." Alisema Dkt. Asiedu.
Kwa uzinduzi huu, Ecobank Tanzania inaendelea kuwa kinara katika kuhimiza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake kupata nyenzo, maarifa na mitaji itakayowawezesha kustawi katika biashara.

Tanzania’s Mineral Sector Opportunities Highlighted at Geita Gold Fair ✨

 








Commissioner of the Mining Commission, Dr. Theresia Numbi, together with CPA Venance Kasiki, Director of Mineral Audit and Trade, shared valuable insights on available opportunities for Tanzanians in the mineral sector during the Local Content Forum at the Geita Gold Fair 2025.

The forum, themed “Opportunities and Roles for Mining Service Providers and the Importance of Establishing Local Industries,” brought together key stakeholders to discuss how local investors and miners can actively engage in the sector and contribute to value addition.

Guest of Honour, Chairperson Dr. Janet R. Lekashingo, encouraged participants to seize these opportunities for sustainable growth, while other senior leaders, including Commissioner Engineer Theonestina Mwasha, reinforced the Commission’s commitment to transparency and local participation.

#MiningTanzania #LocalContent #GeitaGoldFair #MineralSector #InvestmentOpportunities

WANABLOGU SASA NI SEHEMU YA FAMILIA YA HABARI NCHINI

  Mwandishi Wetu Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) umeingia rasmi kwenye familia kubwa ya vyombo vya habari baada ya kukabidhiwa hati za...