Friday, November 07, 2025

🔴🔴HIFADHI YA MPANGA-KIPENGERE YAENDELEA KUWA LULU YA VIZAZI VIJAVYO

 






📍Wanafunzi wa Nyanda za Juu Kusini Wapiga Kambi Kujifunza na Kutali 

Na Beatus Maganja, Njombe.

Wahenga walioshiba tunu za uhifadhi na utalii nchini waliwahi kusema "Kama unataka kujua uzuri wa Tanzania tembea ndani ya moyo wake, na moyo huo ni Hifadhi zake". Wengine walisema "Kuna safari ambazo hubadilisha mawazo, na kuna nyingine zinazogusa mwili, nafsi, moyo na roho".

Kuna mahali duniani ambapo miamba huzungumza Kwa sauti ya utulivu, mito ikiimba nyimbo za kale na upepo ukiandika mashairi yasiyofutika juu ya majani ya kijani, mahali ambapo asili huvaa vazi za kizalendo, mahali ambapo historia ikiishi, elimu ikitembea na Tanzania ikitabasamu. Hapa ndipo unapoikuta Hifadhi ya Mpanga-Kipengere, hifadhi iliyopo Mikoa ya Mbeya na Njombe ikiwa chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA.

Leo Novemba 7, 2025 TAWA tulishuhudia ukurasa mwingine mzuri wa historia ya elimu na uhifadhi ulioandikwa ndani ya Hifadhi hii, wakati walimu na wanafunzi wa shule ya Sekondari Lupalilo kutoka Mkoa wa Njombe walipoitembelea Kwa ziara ya kujifunza na kutalii.

Ziara hii si safari ya kawaida, bali mwendelezo wa hamasa inayofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia TAWA inayosisitiza dhana ya "Tumerithishwa Tuwarithishe" lakini pia dhana ya "Tembea Tanzania, Jifunze Tanzania" dhana za utalii wa ndani zilizovuka mipaka ya starehe na kuwa chombo cha elimu, uchumi na uzalendo.

Kwa miaka kadhaa sasa, Shule ya Lupalilo imekuwa mfano wa Kuigwa Kwa kuleta wanafunzi Mpanga-Kipengere, Si Kwa kutazama tu mandhari yake, bali kujifunza Kwa macho, miguu na akili. Mahali ambapo kila mwamba ni somo, kila korongo ni darasa na kila chemichemi ni nukuu ya uumbaji.

Ni Hifadhi pekee nchini ambapo mwanafunzi huweza kushuhudia miamba yote mitatu ya sayansi ya jiolojia. Mwamba moto, mwamba tabaka na mwamba geu.

Lakini Mpanga-Kipengere haizungumzi tu jiolojia, bali ni kitovu cha urithi wa historia ya Tanzania, mahali ambapo bado yanapumua majina makubwa ya Chifu Mkwawa Mkwavinyika na Chifu Merere, mashujaa waliotetea ardhi hii kabla haijawa hifadhi wakiamini kuwa nchi bila heshima ya ardhi yake ni nyumba isiyo na msingi.

Kupitia ziara kama hizi, vijana wanajengewa moyo wa uzalendo, kupenda mazingira na kuthamini rasilimali za taifa. Ni mahali ambapo vizazi vinalelewa si tu kuwa wasomi, bali walinzi wa urithi wa Tanzania.

Kwa maneno mafupi, Hifadhi ya Mpanga-Kipengere ni darasa liliandikwa Kwa mikono ya Muumba mwenyewe, ni darasa la uhai,mahali ambapo kila mgeni huondoka na zawadi inayoonekana Kwa macho ya nyama, zawadi ya kutua msongo wa mawazo na kuongeza upendo Kwa nchi yake, mahali ambapo mgeni huondoka akiwa amebeba zaidi ya kumbukumbu na ndoto mpya, ndoto ya kizazi kinachotambua kuwa utalii ni darasa, na uhifadhi ni urithi.

Karibu Hifadhi ya Mpanga-Kipengere, Hifadhi hii ni salama na atakaye aje

DODOMA RESIDENT MINES OFFICE RELOCATES TO NEW PREMISES


Dodoma, November 7, 2025

The Dodoma Resident Mines Office has announced the relocation of its offices from Kizota to new premises within the Geological Survey of Tanzania (GST) building, located along Kikuyu Avenue near the Post Office.

According to a public notice issued by Engineer Menard Msengi, the Resident Mines Officer, the relocation takes effect from 10th November 2025. 

The new office is conveniently accessible via the road from Nyerere Square through Kikuyu Avenue heading towards the Post Office.

Engineer Msengi assured all Government Institutions, Private Sector Entities, and Mining Stakeholders that all services will continue to be offered as usual at the new location during official working hours, from 7:30 a.m. to 3:30 p.m., Monday to Friday.

He further expressed appreciation for the continued cooperation of stakeholders and apologized for any inconvenience the relocation may cause.

The relocation aligns with the Mining Commission’s vision of becoming a leading institution in the management and regulation of the mineral sector for sustainable development. 

It also supports the Commission’s mission to promote and regulate the mining industry in Tanzania by ensuring transparency, accountability, and value addition for national prosperity. 

The move reflects the Commission’s commitment to its core values of integrity, professionalism, efficiency, teamwork, and customer focus

UHIFADHI NDIO MOYO KATIKA SEKTA YA UTALII; KAMISHNA BADRU.




Na Mwandishi wa NCAA, Karatu.

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) Bw. Abdul-Razaq Badru ameeleza kuwa kusimamia na kuendeleza uhifadhi ni jukumu la msingi kwa mamlaka hiyo  kwani uhifadhi  ndiyo moyo katika ustawi wa utalii na maendeleo ya jamii.

Akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika ofisi za makao makuu Karatu Arusha leo tarehe 7 Novermba, 2025 Kamishna Badru amesisitiza kuwa, usimamizi madhubuti wa rasilimali za wanyamapori, Misitu na Malikale zilizopo hifadhi ya Ngorongoro ni jambo la kufa na kupona na kueleza watumishi hao kuwahudumia wageni wanaotembelea hifadhi kwa wakati, ukarimu, uadilifu na nidhamu ili kuendelea kulinda chapa ya Ngorongoro (Brand) kama eneo bora la utalii wa kifahari (Premium  Safari Destination)

“Jukumu la msingi kwa kila mtumishi wa Ngorongoro ni Uhifadhi kisha mengine yanafuata, uhifadhi na ulinzi wa rasilimali ni jambo la kufa na kupona, hivyo nawasisitiza  kuhakikisha kila mmoja anakuwa mlinzi wa rasilimali hizo.

Akitoa taarifa  ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo Naibu Kamishna  anayeshughulikia uhifadhi,utalii na maendeleo ya jamii Joas Makwati ameeleza kuwa idadi ya watalii imeendelea kuongezeka ambapo robo ya kwanza iliyoishia Septemba 2025 zaidi ya watalii 350,000 wametembelea Ngorongoro. 

Kwa upande wake Naibu Kamishna anayeshughulikia huduma za shirika Aidan Makalla amewataka watumishi kuwa wazi kuchangia maendeleo ya mamlaka kwa kuendelea kutoa ushauri,maoni na Mtazamo katika majukumu ya taasisi ili kuhakikisha huduma zinaendelea kuwa bora na endelevu.

TANZANIA IKO TAYARI KUSHIRIKI MKUTANO MKUBWA WA UTALII DUNIANI




Na Mwandishi Wetu, Riyadh

Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, umefika nchini Saudi Arabia kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 26 wa Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism) unaofanyika mjini Riyadh, kuanzia wiki hii.

Akizungumza na wataalamu wa Tanzania katika kikao cha maandalizi kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Riyadh, Dkt. Abbasi alisema Tanzania iko tayari kushiriki kikamilifu katika mkutano huo muhimu unaojumuisha mawaziri, makatibu wakuu na wadau wakubwa wa utalii kutoka zaidi ya nchi 150 duniani.

“Tanzania ni mwanachama hai wa Shirika hili na ni miongoni mwa nchi wachache zinazoshiriki katika Kamati ya Utendaji ya UN Tourism, hivyo tunakuja tukiwa na sauti na mchango mahsusi katika mijadala mikubwa kuhusu mustakabali wa sekta ya utalii duniani,” alisema Dkt. Abbasi.

Aliongeza kuwa mkutano huo ni fursa muhimu kwa Tanzania kuonyesha mafanikio yake katika kukuza sekta ya utalii, hususan kupitia kampeni za kimkakati kama “Tanzania Unforgettable” na utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa kinara wa diplomasia ya uchumi kupitia utalii.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi, pamoja na ajenda kuu za kikao, moja ya mambo muhimu yatakayojadiliwa ni uchaguzi wa Katibu Mkuu mpya wa UN Tourism, atakayeanza kazi rasmi Januari 2026, kuchukua nafasi ya uongozi wa sasa na kuendeleza mageuzi katika sekta hiyo duniani.

Aidha, ujumbe wa Tanzania utashiriki pia katika mikutano ya kando (side events) itakayohusisha majadiliano ya uwekezaji, ubunifu, matumizi ya teknolojia katika utalii, na uendelevu wa mazingira – maeneo ambayo Tanzania imepiga hatua kubwa kwa miaka ya karibuni.

Dkt. Abbasi alisisitiza kuwa Tanzania inaingia katika mkutano huo ikiwa na dhamira ya kuimarisha ushirikiano na wadau wa kimataifa, kuvutia wawekezaji, na kuongeza idadi ya watalii kutoka mataifa mbalimbali, hasa kutoka Mashariki ya Kati, Asia, na Ulaya.

“Lengo letu ni kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kinara wa utalii wa asili na kipekee barani Afrika, tukitumia vivutio vyetu vya kimataifa kama Hifadhi ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, na Visiwa vya Zanzibar kama nyenzo za kiuchumi na diplomasia,” aliongeza.

Mkutano huo wa 26 wa Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism General Assembly) unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki hii, ukitoa dira mpya ya kimataifa ya kukuza utalii endelevu, ujumuishi, na unaolenga maendeleo ya watu.

Thursday, November 06, 2025

RAIS SAMIA AKUTANA NA MJUMBE MAALUM WA RAIS WA URUSI IKULU CHAMWINO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Sergei Kiriyenko, Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin uliowasilishwa kwake na Mhe. Sergei Kiriyenko, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 06 Novemba, 2025.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Sergei Kiriyenko, Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin, leo tarehe 06 Novemba 2025, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

Mhe. Dkt. Samia alipokea kwa heshima ujio wa Mhe. Kiriyenko mara alipowasili Ikulu, ambapo viongozi hao walipata nafasi ya kubadilishana mawazo na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi.

Mazungumzo yao yalilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii uliopo kati ya mataifa haya mawili, hususan katika maeneo ya uwekezaji, elimu, nishati na teknolojia.

Ziara hiyo ni ishara ya kuimarika kwa mahusiano ya kihistoria kati ya Tanzania na Urusi, huku serikali zote mbili zikiahidi kuendelea kushirikiana katika kuleta maendeleo endelevu kwa manufaa ya wananchi wa nchi zao.

#IkuluChamwino #RaisSamia #TanzaniaUrusi #DiplomasiaYaMaendeleo #BuildingPartnerships #Dodoma

Sunday, October 26, 2025

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) ukiongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye, Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na ujumbe wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) ukiongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye, Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025. FP-ICGLR ni miongoni mwa misheni mbalimbali zilizowasili nchini kwa ajili ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Uganda, Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe mara baada ya mazungumzo, Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ulioongozwa na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Uganda, Dkt. Speciosa Wandira Kazibwe Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha Tuzo ya Presidential Global Water Changemakers 2025 ambayo alitunukiwa tarehe 13 Agosti, 2025 Cape Town, nchini Afrika Kusini. Tuzo hiyo iliwasilishwa kwake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, Ikulu Tunguu Zanzibar tarehe 26 Oktoba, 2025. Tuzo hiyo ya Ulimwengu ya Marais wanaoleta Mabadiliko katika Sekta ya Maji imetolewa kwa kutambua uongozi bora na dhamira ya dhati katika kuanzisha na kuendeleza mipango na miradi ya Maendeleo katika Sekta ya maji nchini Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 26 Oktoba 2025, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR), ukiongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mheshimiwa Domitien Ndayizeye, katika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar.

Mazungumzo hayo yalijikita katika masuala ya demokrasia, amani na ushirikiano wa kikanda, huku ujumbe huo ukiwa miongoni mwa misheni mbalimbali ya kimataifa iliyowasili nchini kwa ajili ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025.

Rais Dkt. Samia aliukaribisha ujumbe huo kwa ukarimu na kueleza kuwa Tanzania imejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, uwazi na kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na utawala bora. Aidha, alisisitiza kuwa Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha hali ya usalama inabaki kuwa shwari katika kipindi chote cha uchaguzi.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Domitien Ndayizeye alitoa pongezi kwa Tanzania kwa maandalizi mazuri ya uchaguzi na kwa kuendeleza utamaduni wa kisiasa wa amani na umoja unaoitambulisha nchi hiyo katika ukanda wa Maziwa Makuu.

Ameeleza kuwa FP-ICGLR, kama taasisi ya kikanda inayojikita katika kukuza demokrasia na utawala bora, itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha michakato ya kisiasa inatekelezwa kwa misingi ya haki, ushirikishwaji na utulivu.

Mazungumzo hayo yanaendelea kuonyesha dhamira ya Tanzania katika kushirikiana na jumuiya za kikanda na kimataifa katika kulinda amani, demokrasia na maendeleo endelevu barani Afrika.

#RaisSamia #FPICGLR #Uchaguzi2025 #TanzaniaInajengaDemokrasia #AmaniNaUmoja #Zanzibar

 

RAIS DKT. MWINYI AKUTANA NA MISHENI YA UANGALIZI WA UCHAGUZI YA UMOJA WA AFRIKA
















Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, leo amefanya mazungumzo na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Umoja wa Afrika (AUEOM), ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Masisi, Ikulu Zanzibar. Mheshimiwa Masisi aliambatana na ujumbe wa maafisa waandamizi kutoka AUEOM walioko nchini kwa ajili ya kufuatilia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais Dkt. Mwinyi aliwakaribisha wageni hao na kuwapongeza kwa hatua ya Umoja wa Afrika kutuma timu ya waangalizi kama sehemu ya kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi, amani na kwa kuzingatia misingi ya demokrasia barani Afrika.

Ameeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha mazingira yote ya uchaguzi yanabaki kuwa salama na yenye amani, akisisitiza kuwa Zanzibar imejipanga vyema kwa zoezi hilo muhimu la kidemokrasia. “Hali ya ulinzi na usalama ni shwari, na wananchi wako tayari kushiriki kikamilifu katika uchaguzi,” alisema Rais Mwinyi.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali inaendelea kushirikiana kwa karibu na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha taratibu zote za uchaguzi zinafuatwa kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wao, ujumbe wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Umoja wa Afrika (AUEOM) umepongeza hatua za maandalizi zilizochukuliwa na Serikali ya Zanzibar, hususan katika kuhakikisha mjumuisho wa makundi maalum ya jamii kama vile wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika mchakato wa uchaguzi.

Viongozi hao wamesema kuwa Umoja wa Afrika unaendelea kufuatilia mwenendo wa maandalizi ya uchaguzi nchini Tanzania kwa lengo la kuhakikisha chaguzi zinazoendeshwa barani Afrika zinakuwa huru, haki na zenye uwazi. Wameongeza kuwa ni matarajio yao kuwa uchaguzi wa mwaka huu, Tanzania Bara na Zanzibar, utaendelea kuwa mfano wa kuigwa kwa nchi nyingine katika kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Mheshimiwa Masisi aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ukarimu na ushirikiano walioupata tangu walipowasili, akisisitiza kuwa ujumbe wake una imani kubwa na dhamira ya Tanzania ya kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa amani na kufanyika kwa misingi ya sheria na taratibu zote husika.

Mazungumzo hayo ni sehemu ya ratiba ya mikutano ya Misheni hiyo ya AUEOM na viongozi mbalimbali nchini, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ufuatiliaji wa mchakato mzima wa uchaguzi wa mwaka 2025

🔴🔴HIFADHI YA MPANGA-KIPENGERE YAENDELEA KUWA LULU YA VIZAZI VIJAVYO

  📍Wanafunzi wa Nyanda za Juu Kusini Wapiga Kambi Kujifunza na Kutali  Na Beatus Maganja, Njombe. Wahenga walioshiba tunu za uhifadhi na ut...