Mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika
 akitoka katika ukumbi wa Bunge la Tanzania leo mjini Dodoma baada ya 
kukataa kufuta kauli ya kumdhalilisha Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa 
Tanzania kuwa dhaifu. Mbunge huyo alitoa kauli hiyo wakati akichangia 
Bajeti ya serikali ya mwaka 2012/13 katika mkutano unaoendelea.
(Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dodoma) 
  
Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika akiteta na Mbunge wa jimbo la Wawi
 Hamad Rashid Mohamed (kushoto) na Mbunge wa Bariadi Mashariki John 
Cheyo  mara baada ya kuondolewa Bungeni leo mjini Dodoma baada ya 
kukataa kufuta kauli ya kumdhalilisha Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa 
Tanzania kuwa dhaifu. Mbunge huyo alitoa kauli hiyo wakati akichangia 
Bajeti ya serikali ya mwaka 2012/13 katika mkutano unaoendelea.

No comments:
Post a Comment