Saturday, January 24, 2015

ALHAJ ALI HASSAN MWINYI NA MHE. EDWARD LOWASSA KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 20 YA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA YA MAASAI, MONDULI

Mbunge wa Monduli na waziri mkuu wa zamani Mh Edward Lowassa na mkewe Mama Regina Lowassa wakimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi na mkewe Mama Sitti Mwinyi  katika sherehe za miaka 20 ya shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai, Jumamosi,24 January Monduli Mlimani, kata ya Engutoto.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Al hadji Ali Hassan Mwinyi akizindua moja ya sanamu za kumbukukumbu ya waanzishi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai ambayo imeadhimisha miaka 20 toka kuanzishwa kwake,huko Monduli Mlimani, jumamosi 24 January.
Mke wa mbunge wa Monduli mama Regina Lowassa akipanda mti wa kumbukumbu ya miaka 20 tokea kuanzishwa kwa shule ya sekondari ya wasichana ya Maasai wilayani Monduli jumamosi January 24.Anayeshuhudia ni mumewe Mh Edward Lowassa na mbunge wa Viti maalum(ccm) mkoa wa Arusha Mhe Namelok Sokoine.

No comments:

KAMISHNA KUJI ATOA WITO TANAPA KUWA NA SACCOS MOJA

Na Edmund Salaho - Tanga Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, CPA Musa Nassoro Kuji ambaye pia ni mlezi wa HIFADHI SACCOS LTD ametoa wito kwa watumi...