Afisa Sheria Mwandamizi wa NHC, Scholastica Kilagane, alitoa elimu ya kina
kuhusu dhana ya hati pacha (Unit title)
MZEE WA MSHITU
Afisa Sheria Mwandamizi wa NHC, Scholastica Kilagane, alitoa elimu ya kina
kuhusu dhana ya hati pacha (Unit title)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Ziara ya Kikazi ya Rais
wa Jamhuri ya Rwanda Mhe. Paul Kagame, Ikulu Jijini Dar es Salaam,
tarehe 03 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo na Ujumbe wa
Rwanda uliongozwa na Rais wa Nchi hiyo Mhe. Paul Kagame, tarehe 03 Mei,
2026.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza mazungumzo ya ngazi ya juu kati ya Tanzania na Rwanda yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 03 Mei 2026, akiwa mwenyeji wa Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame, katika ziara ya kikazi yenye lengo la kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.
Mazungumzo hayo yalijikita katika maeneo muhimu ya ushirikiano ikiwemo biashara, uwekezaji, miundombinu ya kikanda, pamoja na kuimarisha amani na usalama katika ukanda wa Afrika Mashariki. Viongozi hao wawili walisisitiza umuhimu wa kuendeleza mshikamano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Rwanda kwa manufaa ya wananchi wa pande zote.
Baada ya mazungumzo hayo, Rais Samia pia alizungumza na waandishi wa habari ambapo alieleza kuwa ziara hiyo ni ishara ya kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia na nia ya pamoja ya kuharakisha maendeleo ya kikanda kupitia ushirikiano wa karibu zaidi.
Kwa ujumla, ziara ya Rais Paul Kagame nchini Tanzania imeacha alama ya diplomasia yenye nguvu, ikithibitisha dhamira ya viongozi hao wawili kuendeleza ushirikiano wa kimkakati unaolenga ustawi wa wananchi wa Afrika Mashariki.
Mara baada ya kuwasili, Mhe. Kagame alisaini Kitabu cha Wageni Ikulu, ishara ya heshima na uthibitisho wa ziara yake rasmi nchini Tanzania.
Tukio hilo linaakisi umuhimu wa ziara hii katika kukuza ushirikiano wa kimkakati kati ya Rwanda na Tanzania, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji, miundombinu na maendeleo ya kikanda.
Katika picha nyingine, Rais Samia Suluhu Hassan anaonekana akiwa pamoja na mgeni wake Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili Ikulu—taswira inayoonyesha ukaribu wa kidiplomasia na dhamira ya pamoja ya viongozi hawa katika kusukuma mbele ajenda za maendeleo na ustawi wa wananchi wao.
Ziara hii ya kikazi inatarajiwa kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa pande mbili, huku ikiimarisha nafasi ya nchi hizi katika kuchochea ukuaji wa uchumi na mshikamano wa kikanda ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Ryzhenkov amewasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, ambapo alipokewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe, pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Belarus nchini Mhe.Dzmitry Krasouski.
Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Ryzhenkov anatarajiwa kufanya mazungumzo ya pande mbili na mwenyeji wake, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Aprili 28, 2026, jijini Dar es Salaam. Aidha, atakutana na viongozi wengine wa Serikali kwa lengo la kuendeleza na kupanua ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Ziara hiyo inalenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Belarus pamoja na kukuza ushirikiano wa kiuchumi katika maeneo yenye maslahi ya pamoja.

Na. Meleka Kulwa- Fullshangwe Blog, Dodoma
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amesema kuwa Serikali inaendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kuifanya sekta ya madini kuwa injini muhimu ya kukuza uchumi wa Taifa kwa kuwekeza zaidi katika mnyororo wa thamani wa madini mkakati na kuhamasisha uwekezaji katika uongezaji thamani.
Ameyabainisha hayo Aprili 27, 2026 Jijini Dodoma, wakati akiwasilisha bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, amesema kuwa madini mkakati yakiwemo lithium, graphite, nickel, cobalt na rare earth elements yana nafasi kubwa katika maendeleo ya teknolojia za kisasa hususan nishati safi. Aidha amebainisha kuwa mwelekeo wa dunia kutumia teknolojia rafiki kwa mazingira unaongeza mahitaji na thamani ya madini hayo katika soko la kimataifa.
Pia ameongeza kuwa Serikali imejipanga kuimarisha uwekezaji katika utafutaji na uchimbaji wa madini hayo ili kuongeza uzalishaji pamoja na mapato ya Taifa. Amesema kuwa tafiti za masoko mapya zitafanyika ili kupanua wigo wa biashara huku taratibu za utoaji leseni zikirahisishwa kwa wawekezaji.
Amesema kuwa lengo kuu ni kuhakikisha Watanzania wananufaika moja kwa moja kupitia ajira, mapato na maendeleo ya viwanda vinavyotokana na rasilimali hizo.
Aidha amebainisha kuwa Serikali imeweka mkakati wa kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya uchenjuaji, uyeyushaji na usafishaji wa madini ili kuongeza thamani kabla ya kusafirishwa nje ya nchi. Amesema hatua hiyo inalenga kupunguza usafirishaji wa madini ghafi na kuongeza mapato kupitia bidhaa zilizoboreshwa.
Pia ameongeza kuwa eneo la Buzwagi wilayani Kahama limetengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vya kuongeza thamani madini, hatua inayotarajiwa kuvutia wawekezaji na kuongeza ajira kwa wananchi.
Aidha amebainisha kuwa Serikali inaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha viwanda vya usafishaji wa dhahabu vinapata ithibati ya kimataifa ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la dunia.
Amesema kuwa Tanzania inatarajia kuandaa mkutano wa saba wa kimataifa wa uwekezaji katika sekta ya madini utakaofanyika Dar es Salaam mwezi Novemba 2026, ambapo wadau mbalimbali watakutana kujadili fursa na changamoto za sekta hiyo.
Kwa upande wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2025/2026, amesema kuwa Wizara imepiga hatua kubwa ikiwemo kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato na kuimarisha usimamizi wa rasilimali madini.
Aidha amebainisha kuwa Bunge liliidhinisha shilingi bilioni 224.98 kwa ajili ya Wizara, ambapo kati ya hizo shilingi bilioni 100.38 zilitengwa kwa matumizi ya kawaida na shilingi bilioni 124.60 kwa miradi ya maendeleo. Amesema kuwa hadi Machi 2026, Wizara ilikuwa imepokea shilingi bilioni 82.90.
Pia ameongeza kuwa katika ukusanyaji wa maduhuli, Wizara ilipangiwa kukusanya shilingi trilioni 1.41 lakini hadi Machi 2026 tayari ilikuwa imekusanya shilingi trilioni 1.03, sawa na asilimia 114.94 ya lengo la kipindi husika.
Amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na kuimarishwa kwa ukaguzi katika maeneo ya uchimbaji, masoko ya madini, vituo vya ununuzi pamoja na mipaka ya nchi ili kudhibiti upotevu wa mapato.
Aidha amebainisha kuwa thamani ya biashara ya madini imeongezeka na kufikia shilingi trilioni 4.90 katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026 ikilinganishwa na shilingi trilioni 2.82 kwa kipindi kama hicho mwaka uliopita.
Pia ameongeza kuwa Serikali imeendelea kudhibiti utoroshaji wa madini ambapo madini yenye thamani ya shilingi bilioni 3.31 yalikamatwa katika matukio 55 na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Amesema kuwa mapato ya fedha za kigeni yameongezeka ambapo mauzo ya madini nje ya nchi yalifikia dola milioni 5,401.9 mwaka 2025 kutoka dola milioni 4,119.9 mwaka 2024.
Aidha amebainisha kuwa mchango wa sekta ya madini katika Pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 9.1 mwaka 2023 hadi asilimia 10.1 mwaka 2024 na kufikia wastani wa asilimia 11.9 katika robo tatu za mwaka 2025
Mradi wa Masasi Commercial Complex umekabidhiwa rasmi, ukiwa ni alama ya mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya kisasa yenye kuzingatia ubora na thamani kwa jamii.
Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa NHC Mkoa wa Lindi, Omari Malalamangi, aliipongeza timu ya ujenzi kwa kazi kubwa waliyoifanya licha ya changamoto ya maji wakati wa uchimbaji wa msingi.
Alisisitiza kuwa kujituma kwao kumezaa matokeo bora—jengo lenye hadhi linalovutia na kupongezwa na wengi.
Mradi huu umeacha alama chanya kwa jamii, ukitoa ajira kwa wakazi wa Masasi na kunufaisha sekta mbalimbali zikiwemo huduma za maji, umeme, mama lishe pamoja na wauzaji wa vifaa vya ujenzi.
Kwa upande wake, Meneja Usimamizi wa Miradi NHC, Grace Musita, alieleza kuwa ujenzi umefuata taratibu zote za kitaalamu, huku vipimo vya vifaa kama nondo, kokoto na tofali vikifanyika katika maabara ya Mtwara.
Alibainisha kuwa kila hatua ya ujenzi ilisimamiwa kwa ukaribu na wataalamu ili kuhakikisha ubora unazingatiwa kabla ya kuendelea na hatua inayofuata.
Aidha, mradi umefungua fursa kwa wafanyabiashara wa ndani, ambapo baadhi ya kazi kama uwekaji wa milango ya mbao na tiles zilifanywa na mafundi wazawa wa Masasi.
Musita alimshukuru Mkurugenzi Mkuu pamoja na Menejimenti ya NHC kwa ushirikiano uliowezesha kukamilika kwa mradi huu kwa mafanikio.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Madaraka, Kata ya Jida, alieleza furaha yake akisema ujio wa jengo hili umeubadilisha mtaa huo na kuongeza uhai wa shughuli za kijamii na kiuchumi, huku ajira ndogo ndogo zilizotolewa zikichochea vijana wengi kujikwamua kiuchumi.
Hafla ya makabidhiano ilihitimishwa kwa kukata keki, kuashiria rasmi kuwa Masasi Commercial Complex ipo tayari kutumika.
#NHC #MasasiComplex #UjenziBora #MaendeleoYaJamii #Tanzania
Leo, tarehe 23/04/2026 Makumbusho ya Taifa la Tanzania imepokea ugeni maalum kutoka Chuo cha Kijeshi Misri (Egypt War College) walioko katika ziara ya mafunzo.
Ujumbe huo uliongozwa na Meja Jenerali Mohamed Yehia Zakaria Hassan akiambatana na Brigedia Jenerali Islam Sayed Bakry El-Sayed, huku kwa upande wa mwenyeji wao kutoka Tanzania wakiongozwa na Brigedia Jeneral Kamanda Makanya Erassy kutoka JWTZ Tanzania.
Wageni hao walipokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa la Tanzania, Bi. Pendo Gondwe, ambaye aliwakaribisha na kuwapatia maelezo kuhusu dhima ya taasisi hiyo ya Kimkakati katika kuhifadhi, kulinda na kuendeleza urithi wa historia na utamaduni wa Taifa.
Ujumbe huo uliokuwa na lengo la kujifunza ulipata fursa ya kutembelea na kujifunza historia ya Tanzania kupitia vivutio mbalimbali vilivyopo katika Makumbusho, ikiwemo mabaki ya kihistoria, tamaduni za jamii mbalimbali pamoja na hatua za maendeleo ya taifa. Wageni hao walionesha kuvutiwa na ubora wa maonesho na namna historia ya Tanzania inavyoendelea kuhifadhiwa na kuwasilishwa kwa ufanisi.
Akizungumza baada ya ziara hiyo, kiongozi wa ujumbe, Meja Jenerali Mohamed Yehia Zakaria Hassan, alieleza kufurahishwa kwake na kiwango cha maonesho hayo akisema, “ Maonesho ni bora sana na nimefurahishwa kuona mwendelezo wa historia ukiendelea kukua na kuendelezwa"*
Ziara hiyo ni sehemu ya programu ya mafunzo kwa wanafunzi wa Egypt War College, yenye lengo la kuwajengea uelewa mpana kuhusu historia, utamaduni na mifumo ya kijamii ya mataifa rafiki, pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na kidiplomasia kati ya Tanzania na Misri.
Samia Housing Scheme Kawe: nyumba 560, familia tofauti zikiunganishwa na mtindo mmoja wa maisha ya kisasa—ushirikiano, ustaarabu na “moder...