PRETORIA-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Thandi Moraka pembezoni mwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Pretoria Machi 13, 2026.
ARAWAY GROUP TANZANIA
MZEE WA MSHITU
Friday, March 13, 2026
NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI MORAKA JIJINI PRETORIA
PRETORIA-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Thandi Moraka pembezoni mwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Pretoria Machi 13, 2026.
RAIS SAMIA AWASILI PEMBA KWÀ ZIARA YA KIJAMII YA SIKU MBILI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Pemba kwa Ziara ya Kijamii ya siku mbili, tarehe 13 Machi, 2026. Pamoja na mambo mengine, Mheshimiwa Rais atashiriki Iftar ya pamoja na Viongozi na Wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba.
Thursday, March 12, 2026
Rais Samia Akipokea Taarifa Muhimu Kuhusu Hifadhi ya Ngorongoro

Viongozi mbalimbali na Mabalozi wa Nchi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.
Dodoma, 12 Machi 2026 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma, amepokea rasmi Taarifa za Tume ya Rais kuhusu Kutathmini Mgogoro wa Ardhi pamoja na Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu wa Serikali pamoja na Mabalozi wa nchi mbalimbali, ikionyesha umuhimu wa kitaifa na kimataifa wa masuala haya.
Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari, Katibu Mkuu Mstaafu, Mhandisi Musa Iyombe, alikabidhi rasmi ripoti kwa Rais, akiashiria uwajibikaji na uwazi katika kutatua changamoto za makazi na matumizi ya ardhi ndani ya eneo lenye utajiri wa kipekee wa Maliasili.
Vilevile, Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Masuala ya Ardhi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Dkt. Gerald Ndika, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia haki za wananchi sambamba na uhifadhi wa Hifadhi ya Ngorongoro, ili kuhakikisha maendeleo endelevu.
Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi na mabalozi waliohudhuria hafla hiyo, aliweka wazi azma ya Serikali ya kulinda Maliasili, huku ikidumisha haki za wananchi na kukuza maendeleo ya kijamii.
Aliwashukuru watendaji wa Tume kwa kazi yao ya kina na ya uwazi, akisisitiza kuwa ripoti hizi ni nyenzo muhimu kwa maamuzi ya kitaifa yanayolenga ustawi wa jamii na uendelevu wa Hifadhi ya Ngorongoro.
Hafla hiyo ilimalizika kwa picha ya pamoja, ikithibitisha mshikamano wa viongozi wa Serikali, wadau wa kimataifa, na wananchi katika kuhakikisha kuwa Ngorongoro inaendelea kuwa ishara ya ulinzi wa mazingira na maendeleo ya jamii.
Hatua hii inaashiria hatua kubwa mbele katika kulinda ardhi, Maliasili na kuimarisha maisha ya wananchi wa eneo hili lenye hifadhi ya kipekee duniani.
Wednesday, March 11, 2026
USIPIME KIWANJA UACHE PORI! DODOMA YAWAVAA WAMILIKI WALIOLEGEZA
Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itafuta umiliki wa viwanja vyote ambavyo havijaendelezwa ndani ya muda uliowekwa kisheria, na kuvitwaa kwa ajili ya kuvigawa au kuviuza kwa wahitaji wengine kwa mujibu wa taratibu za sheria.
Kauli hiyo imetolewa Machi 11, 2026 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Halmashauri hiyo, Ndugu Dennis Godwe, ambaye amesema lengo ni kuwakumbusha wananchi na taasisi zinazomiliki viwanja ndani ya Jiji la Dodoma kutekeleza wajibu wao wa kuendeleza maeneo hayo kwa wakati.
Ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 (Sura ya 113), mmiliki wa kiwanja anatakiwa kukiendeleza ndani ya kipindi kisichozidi miezi 36 tangu tarehe ya kupewa umiliki. Kushindwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa masharti ya umiliki na kunaweza kusababisha kufutwa kwa hati.
Hata hivyo, Halmashauri imebaini kuwapo kwa matukio ya watu wasiokuwa waadilifu kuvamia viwanja ambavyo havijaendelezwa, kuondoa bikoni na kuanza kufanya maendeleo bila kuwa wamiliki halali. Vitendo hivyo vimesababisha migogoro ya ardhi na usumbufu kwa wamiliki halali pamoja na Halmashauri, huku baadhi ya wananchi wakilazimika kufika ofisini kufuatilia maeneo yao yaliyovamiwa.
Aidha, imeonya dhidi ya tabia ya kuanza ujenzi wa kudumu bila kibali cha ujenzi kutoka Halmashauri, ikisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria. Ujenzi wowote unaofanywa bila kibali utachukuliwa hatua za kisheria, ikiwemo kubomolewa.
Katika kusimamia utekelezaji wa masharti hayo, Halmashauri inaongozwa na Sheria ya Mipangomiji namba 8 ya mwaka 2007, inayosimamia upangaji na maendeleo ya maeneo ya mijini.
TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO, UWEZESHAJI WANAWAKE RIKA ZOTE
Tanzania imeshiriki mkutano uliohusu kufanikisha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake wa rika zote wakiwemo wazee.
Mkutano huo uliofanyika Machi 10, 2025 ni sehemu ya mkutano wa 70 wa Hali ya Wanawake Duniani (CSW 70) ulioanza Machi 09 hadi Machi 19, 2026 jijini New York nchini Marekani.
Lengo la Mkutano huo ni kuieleza dunia mafaniko ya Uwezeshaji Wanawake katika Sekta mbalimbali hasa upatikanaji wa Haki na huduma za Sheria.
Siku ya Pili ya Mkutano huo ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu.
BARAZA LA WAFANYAKAZI PBPA LAHIMIZWA KUWA NA UADILIFU KATIKA KUWAKILISHA MASLAHI YA WATUMISHI
📍Kibaha, Pwani – Machi 11, 2026
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) wametakiwa kuzingatia uadilifu, uwazi na weledi katika kuwasilisha na kushughulikia changamoto za watumishi wanaowawakilisha, ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji kazi wa taasisi.
Wito huo umetolewa leo Machi 11, 2026 na Meneja wa Fedha na Mipango wa PBPA, Bw. Kedron Mbwilo, alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa PBPA wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Pili cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.
Amesema Baraza la Wafanyakazi ni jukwaa muhimu linalounganisha menejimenti na watumishi, hivyo wajumbe wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na uwajibikaji mkubwa ili kuhakikisha masuala ya watumishi yanawasilishwa na kutatuliwa ipasavyo.
“Baraza la Wafanyakazi ni kiunganishi muhimu kati ya menejimenti na watumishi. Ni wajibu wa wajumbe kuwa waadilifu na kuwawakilisha watumishi wenzao kwa weledi mkubwa ili kuongeza tija na ufanisi katika taasisi,” amesisitiza Bw. Mbwilo.
Aidha, amewahimiza watumishi wa PBPA kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na kujituma ili kuunga mkono jitihada za Serikali katika kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, ambayo kwa upande wa sekta ya nishati inalenga kuhakikisha Tanzania inakuwa na upatikanaji wa uhakika wa nishati ya mafuta, miundombinu imara ya mafuta pamoja na usimamizi bora wa rasilimali za petroli.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu wa PBPA, Bw. Matiko Sanawa, amewahimiza wajumbe wa baraza hilo kutumia kikao hicho kama fursa ya kujadili kwa uwazi maoni, mapendekezo na changamoto mbalimbali zitakazochangia kuimarisha uendeshaji wa taasisi.
Amefafanua kuwa kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi kinafanyika kwa mujibu wa matakwa ya kisheria na kwamba, pamoja na mambo mengine, kitajadili taarifa ya utekelezaji wa Mpango Kazi na Bajeti kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Desemba 2026, pamoja na kuwasilishwa kwa rasimu ya Mpango Kazi wa PBPA kwa kipindi cha 2026/2027 hadi 2030/2031 na rasimu ya Bajeti ya PBPA kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
RAIS SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike leo tarehe 11 Machi, 2026, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.
Mtoto huyo aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu Hassan alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, na amekabidhiwa kwa Rais Dkt. Samia na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai.
Akizungumza wakati wa kumkabidhi mtoto huyo, Mkuu wa Wilaya Tukai alisema mtoto huyo aliokotwa tarehe 17 Januari, 2026 akiwa ametelekezwa katika eneo jirani na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega Mjini.
Alieleza kuwa baada ya kupokea taarifa hizo, alishirikiana na Jeshi la Polisi kumchukua mtoto huyo na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio.
Rais Dkt. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpatia malezi, ulinzi na huduma zote muhimu ili akue katika mazingira salama na yenye upendo.
“Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya. Kuliko kumtupa mtoto ni afadhali ukamkabidhi katika mamlaka za kisheria au kituo cha kulelea watoto. Kila mtoto aliyezaliwa ni hazina, na hatuijui kesho yake,” alisema Rais Dkt. Samia.
NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI MORAKA JIJINI PRETORIA
PRETORIA-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. . Picha na Jube Tranqu...









.jpeg)









.jpeg)







.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)







