Na OWM – TAMISEMI, Arusha
Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini wanaendelea kunufaika moja kwa moja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, hatua inayobadilisha kwa kasi hali ya upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii na kuboresha maisha yao kwa ujumla.
Akizungumza Aprili 22, 2026 jijini Arusha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema hatua ya Serikali chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupeleka fedha nyingi kwenye halmashauri imekuwa na matokeo chanya yanayoonekana moja kwa moja kwa wananchi.
Amesema kupitia uwekezaji huo, wananchi sasa wanashuhudia maboresho katika sekta za afya, elimu, miundombinu na huduma nyingine za kijamii, hali inayorahisisha upatikanaji wa huduma na kuongeza ustawi wa jamii.
“Mafanikio haya yanaonekana wazi kwa wananchi—kuanzia upatikanaji wa huduma bora za afya, mazingira mazuri ya kujifunzia kwa wanafunzi, hadi kuboreshwa kwa miundombinu inayorahisisha shughuli za kiuchumi,” ameeleza Prof. Shemdoe.
Katika hatua nyingine, amewataka viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanaendeleza kasi hiyo kwa kusimamia miradi kwa ufanisi na kuhakikisha inakidhi mahitaji halisi ya wananchi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji, weledi na ushirikiano kati ya viongozi na watendaji ili kuhakikisha manufaa ya miradi hiyo yanaendelea kuwafikia wananchi kwa kiwango kikubwa zaidi.
Kauli hiyo imetolewa kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kufungua Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Viongozi wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), unaofanyika Aprili 22 hadi 23, 2026 jijini Arusha.

.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)
















.jpeg)











.jpeg)


