Saturday, March 14, 2026

Rais Samia atoa Bilioni 15 Maboresho Shule ya Polisi Kilimanjaro








Na Mwandishi Wetu,Kilimanjaro

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan ametoa  Shilingi Bilioni 25 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa Kikao cha Maafisa Wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi kilichofanyika mwaka 2024 lengo ikiwa kuifanyia maboresho Shule cha Polisi Kilimanjaro ambacho kinakabiliwa na uchakavu wa Majengo ambayo yalijengwa tangu  mwaka 1933 ambapo yanajumuisha Mabweni ya Wanafunzi,Madarasa na Nyumba za Askari.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama(NUU) iliyotembelea shule hiyo kukagua matumizi ya fedha hiyo iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ikiwa ni utaratibu wa Kamati za Bunge kufuatilia matumizi ya fedha zinazotolewa na serikali kwa miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Leo tunazungumza Wizara ya Mambo ya Ndani ambapo Rais ameweza kuyafanya haya ambayo wajumbe mmeyashuhudia leo kwa kiasi cha Shilingi Bilioni 25 ambazo mmeona kwa kiwango kikubwa na uweledi mkubwa wa jeshi katika utekelezaji na uwezo wa kusimamia kazi.Kwa kweli hatuna namna ya kuweza kumshukuru Mheshimiwa Rais Zaidi ya kumuombea afya njema,umri na rizki ili Mwenyenzi Mungu aendelee kumpa hekima na busara ili sisi wizara tuendelee kuwa wanufaika wa uongozi wake” amesema Waziri Katambi

“Lakini tuna miradi ya ujenzi wa nyumba sehemu mbalimbali ambapo Mheshimiwa Rais pia anatoa kiasi kikubwa cha fedha na pale Dodoma tayari mradi ushaanza na tunatumia wataalamu wetu wa ndani na wanajenga kwa viwango vile vile kama mlivyoona hapa Shule ya Polisi,tunaenda kufanya maboresho ya maslahi kwa askari,mabadiliko ya sera na sheria  na teknolojia za kisasa pia zinaendelea kuingizwa jeshini ili vifaa vya kisasa vitumike katika kulinda usalama wetu.” aliongeza Waziri Katambi

Akizungumza katika ziara hiyo,Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya NUU, Najma Murtaza Giga, ametoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa kujenga mradi huo kwa ufanisi na uweledi mkubwa huku akikiri kuona thamani ya kiasi cha fedha kilichotolewa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan huku akiweka wazi Kamati kuendelea  kuwa na imani na Jeshi la Polisi katika masuala mbalimbali na hivyo haina budi kuendelea kulisemea Jeshi la Polisi kuhakikisha linawezeshwa ili liweze kutekeleza majukumu yake ya kulinda usalama wa raia na mali zao kwa weledi na ufanisi wa hali ya juu.

Nae Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, ameishukuru Kamati hiyo ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) kwa kutenga muda na kuona umuhimu wa kutembelea Shule ya Polisi Tanzania-Moshi mkoani Kilimanjaro na kuona thamani ya fedha iliyotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inavyotumika kwa kuhakikisha ubora na ufanisi unaonekana kwenye miradi hiyo ya ujenzi.

Aidha, IGP Wambura, ameiambia kamati hiyo kuwa, serikali ya awamu ya sita imeendelea kuliwezesha Jeshi la Polisi kwenye miundombinu mbalimbali kote nchini ili kuhakikisha askari Polisi wanafanya kazi kwenye mazingira mazuri na wezeshi katika kuwahudumia wananchi, kutatua kero mbalimbali ili waendelee kufanya kazi zao bila uwepo wa matishio ya kihalifu nchini.

Friday, March 13, 2026

NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI MORAKA JIJINI PRETORIA

 








PRETORIA-Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Thandi Moraka pembezoni mwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Pretoria Machi 13, 2026.

Mazungumzo hayo ambayo yalihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Fedha. Mhe. Laurent Luswetula na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. James Bwana yalijadili namna bora ya kuimarisha uhusiano na ushiririkiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Afrika Kusini, nchi ambazo zina uhusiano wa kihistoria wa muda mrefu.
Moja ya hatua ambazo viongozi hao wamekubaliana ni kuongeza kasi ya kukamilisha rasimu za Hati za makubaliano katika maeneo mbalimbali ili ziweze kusainiwa na kutekelezwa kwa manufaa ya pande zote mbili.
Mhe. Maghembe alipongeza nchi ya Afrika Kusini kwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa nchi 20 tajiri zaidi duniani (G20) mwaka 2025 na maandalizi mazuri ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri la SADC uliofanyika kwa siku mbili Machi 12 na 13, 2026.

RAIS SAMIA AWASILI PEMBA KWÀ ZIARA YA KIJAMII YA SIKU MBILI


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Pemba kwa Ziara ya Kijamii ya siku mbili, tarehe 13 Machi, 2026. Pamoja na mambo mengine, Mheshimiwa Rais atashiriki Iftar ya pamoja na Viongozi na Wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba.










Thursday, March 12, 2026

Rais Samia Akipokea Taarifa Muhimu Kuhusu Hifadhi ya Ngorongoro

Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Katibu Mkuu Mstaafu, Mhandisi Musa Iyombe akizungumza na kukabidhi Taarifa ya Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.
Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Masuala ya Ardhi katika Wilaya ya Ngorongoro, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Dkt. Gerald Ndika akizungumza na kukabidhi Taarifa ya Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Viongozi mbalimbali mara baada ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 12 Machi, 2026.
Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka akizungumza katika hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.

Viongozi mbalimbali na Mabalozi wa Nchi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.


Viongozi mbalimbali na Mabalozi wa Nchi mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya kupokea Taarifa za Tume ya Rais ya Kutathmini Mgogoro wa Ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma, tarehe 12 Machi, 2026.


Dodoma, 12 Machi 2026 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma, amepokea rasmi Taarifa za Tume ya Rais kuhusu Kutathmini Mgogoro wa Ardhi pamoja na Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu wa Serikali pamoja na Mabalozi wa nchi mbalimbali, ikionyesha umuhimu wa kitaifa na kimataifa wa masuala haya.

Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari, Katibu Mkuu Mstaafu, Mhandisi Musa Iyombe, alikabidhi rasmi ripoti kwa Rais, akiashiria uwajibikaji na uwazi katika kutatua changamoto za makazi na matumizi ya ardhi ndani ya eneo lenye utajiri wa kipekee wa Maliasili. 

Vilevile, Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kutathmini Masuala ya Ardhi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Dkt. Gerald Ndika, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia haki za wananchi sambamba na uhifadhi wa Hifadhi ya Ngorongoro, ili kuhakikisha maendeleo endelevu.

Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na viongozi na mabalozi waliohudhuria hafla hiyo, aliweka wazi azma ya Serikali ya kulinda Maliasili, huku ikidumisha haki za wananchi na kukuza maendeleo ya kijamii. 

Aliwashukuru watendaji wa Tume kwa kazi yao ya kina na ya uwazi, akisisitiza kuwa ripoti hizi ni nyenzo muhimu kwa maamuzi ya kitaifa yanayolenga ustawi wa jamii na uendelevu wa Hifadhi ya Ngorongoro.

Hafla hiyo ilimalizika kwa picha ya pamoja, ikithibitisha mshikamano wa viongozi wa Serikali, wadau wa kimataifa, na wananchi katika kuhakikisha kuwa Ngorongoro inaendelea kuwa ishara ya ulinzi wa mazingira na maendeleo ya jamii

Hatua hii inaashiria hatua kubwa mbele katika kulinda ardhi, Maliasili na kuimarisha maisha ya wananchi wa eneo hili lenye hifadhi ya kipekee duniani.

Wednesday, March 11, 2026

USIPIME KIWANJA UACHE PORI! DODOMA YAWAVAA WAMILIKI WALIOLEGEZA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itafuta umiliki wa viwanja vyote ambavyo havijaendelezwa ndani ya muda uliowekwa kisheria, na kuvitwaa kwa ajili ya kuvigawa au kuviuza kwa wahitaji wengine kwa mujibu wa taratibu za sheria.

Kauli hiyo imetolewa Machi 11, 2026 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Halmashauri hiyo, Ndugu Dennis Godwe, ambaye amesema lengo ni kuwakumbusha wananchi na taasisi zinazomiliki viwanja ndani ya Jiji la Dodoma kutekeleza wajibu wao wa kuendeleza maeneo hayo kwa wakati.

Ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 (Sura ya 113), mmiliki wa kiwanja anatakiwa kukiendeleza ndani ya kipindi kisichozidi miezi 36 tangu tarehe ya kupewa umiliki. Kushindwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa masharti ya umiliki na kunaweza kusababisha kufutwa kwa hati.

Hata hivyo, Halmashauri imebaini kuwapo kwa matukio ya watu wasiokuwa waadilifu kuvamia viwanja ambavyo havijaendelezwa, kuondoa bikoni na kuanza kufanya maendeleo bila kuwa wamiliki halali. Vitendo hivyo vimesababisha migogoro ya ardhi na usumbufu kwa wamiliki halali pamoja na Halmashauri, huku baadhi ya wananchi wakilazimika kufika ofisini kufuatilia maeneo yao yaliyovamiwa.

Aidha, imeonya dhidi ya tabia ya kuanza ujenzi wa kudumu bila kibali cha ujenzi kutoka Halmashauri, ikisisitiza kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria. Ujenzi wowote unaofanywa bila kibali utachukuliwa hatua za kisheria, ikiwemo kubomolewa.

Katika kusimamia utekelezaji wa masharti hayo, Halmashauri inaongozwa na Sheria ya Mipangomiji namba 8 ya mwaka 2007, inayosimamia upangaji na maendeleo ya maeneo ya mijini.

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO, UWEZESHAJI WANAWAKE RIKA ZOTE









Tanzania imeshiriki mkutano uliohusu kufanikisha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake wa rika zote wakiwemo wazee.

Mkutano huo uliofanyika Machi 10, 2025 ni sehemu ya mkutano wa 70 wa Hali ya Wanawake Duniani (CSW 70) ulioanza Machi 09 hadi Machi 19, 2026 jijini New York nchini Marekani.

Lengo la Mkutano huo ni kuieleza dunia mafaniko ya Uwezeshaji Wanawake katika Sekta mbalimbali hasa upatikanaji wa Haki na huduma za Sheria.

Siku ya Pili ya Mkutano huo ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu.



BARAZA LA WAFANYAKAZI PBPA LAHIMIZWA KUWA NA UADILIFU KATIKA KUWAKILISHA MASLAHI YA WATUMISHI





📍Kibaha, Pwani – Machi 11, 2026

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) wametakiwa kuzingatia uadilifu, uwazi na weledi katika kuwasilisha na kushughulikia changamoto za watumishi wanaowawakilisha, ili kuongeza ufanisi na tija katika utendaji kazi wa taasisi.

Wito huo umetolewa leo Machi 11, 2026 na Meneja wa Fedha na Mipango wa PBPA, Bw. Kedron Mbwilo, alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa PBPA wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Pili cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.

Amesema Baraza la Wafanyakazi ni jukwaa muhimu linalounganisha menejimenti na watumishi, hivyo wajumbe wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na uwajibikaji mkubwa ili kuhakikisha masuala ya watumishi yanawasilishwa na kutatuliwa ipasavyo.

“Baraza la Wafanyakazi ni kiunganishi muhimu kati ya menejimenti na watumishi. Ni wajibu wa wajumbe kuwa waadilifu na kuwawakilisha watumishi wenzao kwa weledi mkubwa ili kuongeza tija na ufanisi katika taasisi,” amesisitiza Bw. Mbwilo.

Aidha, amewahimiza watumishi wa PBPA kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na kujituma ili kuunga mkono jitihada za Serikali katika kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, ambayo kwa upande wa sekta ya nishati inalenga kuhakikisha Tanzania inakuwa na upatikanaji wa uhakika wa nishati ya mafuta, miundombinu imara ya mafuta pamoja na usimamizi bora wa rasilimali za petroli.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu wa PBPA, Bw. Matiko Sanawa, amewahimiza wajumbe wa baraza hilo kutumia kikao hicho kama fursa ya kujadili kwa uwazi maoni, mapendekezo na changamoto mbalimbali zitakazochangia kuimarisha uendeshaji wa taasisi.

Amefafanua kuwa kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi kinafanyika kwa mujibu wa matakwa ya kisheria na kwamba, pamoja na mambo mengine, kitajadili taarifa ya utekelezaji wa Mpango Kazi na Bajeti kwa kipindi cha Julai 2025 hadi Desemba 2026, pamoja na kuwasilishwa kwa rasimu ya Mpango Kazi wa PBPA kwa kipindi cha 2026/2027 hadi 2030/2031 na rasimu ya Bajeti ya PBPA kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Rais Samia atoa Bilioni 15 Maboresho Shule ya Polisi Kilimanjaro

Na Mwandishi Wetu,Kilimanjaro Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan ametoa  Shilingi Bilioni 25 ikiwa ni utekeleza...