Monday, February 15, 2016

WAZIRI UMMY APOKEA VIFAA KATIKA WODI YA AFYA YA UZAZI YA MAMA NA MTOTO MUHIMBILI

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akipokea vifaa kutoka kwa Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa yaTaifa Lauren Rugambwa Bwanakunu vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Hospitali ya Muhimbili Prof Lawerence Mseru na nayefata ni katibu Mkuu wa wizara hiyo Mpoki Ulisubisya .

Na Raymond Mushumbusi  MAELEZO

Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu amepokea vifaa vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya  Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni agizo la Mhe.Rais alililolitoa mapema mwishoni wa wiki iliyopita katika kuhakikisha kuwa wakinamama wanaojifungua hawalali chini.

Akipokea vifaa hivyo  Mhe. Ummy Mwalimu amesema anamshukuru sana Mhe Rais kwa kuona changamoto hii ya wakina mama kulala chini wakati wakitoka kujifungua na kumuahidi Mhe. Rais kusilimamia vyema suala hilo na kuwaagiza wakurugenzi husika kumpa taarifa ya kuhusu vitanda na magodoro katika Hospitali zote zilizo chini ya wizara yake.

“ Kuanzia sasa sitolala na natuma salamu kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwa fursa hii ni wajibu wao kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya afaya hasa katika vifaa hususan vitanda na magodoro ili kupunguza tatizo hili la wagonjwa katika Hospitali zetu kulala chini wakati tuna uwezo wa kupata vitanda na magodoro”

‘”Mhe.Rais amenifundisha na ametufundisha sote kwamba  kutatua jambo sio mpaka mkae vikao au semina ili kujadili  ila inawezekana kama mkiweka nia ya kulifanya jambo hilo na kuachana na zile kauli za tunalifanyia kazi, tupo katika michakato na kauli kama hizo zisizotatua tatizo kwa wakati unaotakiwa”alisema Ummy.

Bohari ya Dawa ya Taifa imekabidhi jumla ya vitanda 120, Magodoro 120, Mashuka 480, vitanda vya kuzalishia 10,vitanda 10 vya kulaza watoto ambao hawajatimia Njiti  na jumla ya vifaa vyote vina thamani ya shilling Million 100.

Uaandaaji wa wodi hiyo ya akimama wanaojifungua katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umekuja baada ya agizo la Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuli alilolitoa hivi karibuni alipokuwa akiongea na wazee wa Mkoa wa Dar es Salam na kutoa siku mbili kwa wizara Ya Afya kuhamisha ofisi zilizokuwepo za kitengo Afya ya uzazi ya  Mama na Mtoto na kuifanya kuwa wodi ya akina mama ili kupunguza tatizo la kulala chini kwa akina mama wanaotoka kujifungua.

No comments: