Friday, February 19, 2016

UKATAJI WA TIKECT KWA AJILI YA KUANGALIA MECHI UWANJA WA TAIFA KWA NJIA YA ELEKRONIKI WAIVA

tik1
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura ((wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa TFF, BMT na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo mara baada ya kumaliza  wa kikao  kilichofanyika ofisinii kwake leo jijini Dar es Salaam.Kikao hicho kimefanyika ili ya kujadili suala la matumizi ya mashine za Elekroniki katika kukusanya mapato yatokanayo na mauzo ya Tiketi wakati wa mechi kwenye uwanja wa Taifa.
Picha na: Frank Shija, WHUSM
tik2
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura akizungumza katika kikao baina yake na uongozi kutoka TFF na BMT ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kujadili suala la matumizi ya mashine za Elekroniki katika kukusanya mapato yatokanayo na mauzo ya Tiketi wakati wa mechi kwenye Uwanja wa Taifa.Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Dioniz Malinzi na kulia ni Meneja wa Uwanja wa Taifa Rish Urio.
tik3
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura akifuatilia maelezo kutoka kwa Muhasibu Mkuu wa Wizara  hiyo Bibi. Rose Janeth Bandisa (kulia) wakati wa kikao  baina yake na uongozi kutoka TFF na BMT ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.Kikao hicho kimefanyika ili ya kujadili suala la matumizi ya mashine za Elekroniki katika kukusanya mapato yatokanayo na mauzo ya Tiketi wakati wa mechi kwenye Uwanja wa Taifa.Katikati ni Meneja wa Uwanja wa Taifa Rish Urio.
tik4
Katibu Mkuu wa TFF Celestine Mwesiga (kushoto) na Muhasibu Mwandamizi wa TFF Bw. Daniel Msangi wakifuatilia kwa makini wakati wa kikao baina yao na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
tik5
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) akizungumza katika kikao baina ya  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (katikati) na uongozi kutoka TFF na BMT leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Meneja wa Uwanja wa Taifa Rish Urio.
tik6
Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Mohamed Kiganja akizungumza  wakati wa  kikao baina ya  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (katikati) na uongozi kutoka TFF na BMT leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT)

No comments: