Tuesday, October 08, 2013

NHC kuuza nyumba 2,000 za gharama nafuu Oktoba

Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC, David Shambwe akizungumza katika mkutano huo na vyombo vya habari
Waandishi wa habari wakifuatilia kwa kina mkutano huo jini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu katika mahojiano na ITV
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu katika mahojiano na ITV
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo Pichani) kuhusu kampeni hiyo ya mauzo
Mkurugenzi Mkuu Bw. Nehemia Kyando Mchechu amezindua kampeni ya uuzaji wa nyumba za gharama nafuu ambao umebebwa na kauli mbiu iitwayo “NYUMBA YAKO, MAISHA YAKO”. 

Kupitia kampeni hii, Mkurugenzi Mkuu alisema Shirika limezindua rasmi programu ya ujenzi wa nyumba 5,000 (elfu tano). Kampeni imezinduliwa Oktoba tatu mwaka huu.

Alifafanua kuwa kampeni ni ya muda mrefu na imelenga uzinduzi wa uuzaji wa nyumba za gharama nafuu. Alisema kuwa katika awamu ya kwanza Shirika limeanza na nyumba (2,000) elfu mbili ambazo zimefikia katika hatua tofauti ya ujenzi.

Maeneo yaliyoanza kunufaika na mpango huu ni pamoja na Mvomero (Morogoro), Mkinga (Tanga), Lindi, Mkuzo (Ruvuma), Bombambili (Geita), Mlole (Kigoma), Ilembo (Katavi), Kongwa (Dodoma), Unyankumi (Singida), Kibada ( Dar Es Salaam) na Mrara (Babati). 

Uzinduzi huu umekuwa wa aina yake kwa kuwa kabla ya Mkurugenzi Mkuu kuzungumza na Wanahabari, Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Biashara Bw. David Shambwe alifanya semina fupi na Wanahabari ili kufafanua juhudi zinazofanywa na Shirika katika ujenzi wa  miradi ya gharama nafuu na pia changamoto mbalimbali zilizopo katika ujenzi huo. 

Bw. Shambwe alichukua nafasi hii kuwafahamisha Wanahabari kuwa mauzo ya nyumba hizo yataanza rasmi tarehe 13 Oktoba 2013. Lengo ni kuwaandaa wanunuzi ili itakapofika tarehe 13 Oktoba wawe wamejiandaa kununua nyumba hizo. Shirika litaufahamisha umma wa Tanzania kupitia vyombo vya habari.

No comments: