Wednesday, September 24, 2025

Dkt. Samia Akiweka Shada la Maua Kaburini kwa Hayati Mkapa, Lupaso




Mtwara – Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, huko Lupaso, wilayani Masasi, mkoani Mtwara. Tukio hilo limefanyika tarehe 24 Septemba, 2025.

Dkt. Samia aliongozana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali, katika tukio lililobeba kumbukumbu ya heshima na kutambua mchango mkubwa wa Hayati Mkapa katika kuijenga Tanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Mazingira ya tukio yaligubikwa na unyenyekevu, ukitoa taswira ya mshikamano wa kitaifa na dhamira ya kuenzi urithi wa viongozi waliolitumikia taifa kwa dhati.

Kwa kuweka shada hilo la maua, Dkt. Samia alionesha kuendeleza desturi ya heshima na kuthamini misingi iliyowekwa na marais waliotangulia katika kudumisha mshikamano wa Watanzania na mustakabali wa taifa.

No comments:

TRENI YA MWENDOKASI KUFIKA MWANZA 2028

  Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kutoka kulia),akizungumza baada ya kukagua daraja la kupitisha magari chn ya reli, l...