Monday, December 22, 2014

WAZIRI WA HABARI VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO. AKABIDHI ZAWADI KWA MCHEZAJI BORA WA KIKE KATIKA MASHINDANO YA COPA COCA COLA

001Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara(MB) akikagua timu za Vijana waliochini ya miaka 15 kutoka Kinondoni na Dodoma ambazo zilishiriki hatua ya fainali katika mashindano ya Copa Coca Cola mwishoni mwa wikiendi katika uwanja wa Krume jijini Dar es Salaam. Ambapa katika fainali hizo kwa upande wanaume toimu kutoka Dodoma iliibuka bingwa wa mashindano hayo kwa kuichapa Kinondoni jumla ya magoli 4 -0, wakati kwa upande wa wanawake Kinondoni ilinyakua ubingwa kuifunga Ilala kwa mikwaju ya penati 2 – 1 baada ya dakika tisni kumaliza kwa sare ya mbili mbili.
002
3Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) (wa tatu kutoka kushoto) akifurahia mara baada ya kukabidhi zawadi ya mchezaji bora wa kike katika mashindano ya Copa Coca Cola kwa Golikipa wa timu ya Kinondoni Zubeda Mohamed (15). Wakwanza kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Coca Cola Bw. Godfrey Njowoka, Rais wa TFF Jamal Malinzi na nyuma ya waziri anayecheka ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leonard Thadeo.
00Mashabiki wakifuatilia fainali za Copa Coca Cola 2014
003
Wachezaji wa timu ya Dodoma wakifurahia baada ya kukabidhiwa zawadi zao za ubingwa wa michuano ya Copa Coca Cola baada ya kuibuka mabingwa wa mashindano hayo kwa mwaka 2014 kwa mashindano hayo kwa kuichapa Kinondoni jumla ya magoli 4 -0, wakati kwa upande wa wanawake Kinondoni ilinyakua ubingwa kuifunga Ilala kwa mikwaju ya penati 2 – 1 baada ya dakika tisni kumaliza kwa sare ya mbili mbili.
Picha na Frank Shija, WHVUM

No comments: