Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba akiagana na Balozi
wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Eunje Ahn, baada ya mkutano kati
yao kuhusu ushirikiano wa maendeleo, uliofanyika Ofisi Ndogo za Wizara
ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao chake na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Eunje Ahn (hayupo pichani), kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban na kulia ni Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Melckzedeck Mbise, kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba akiongoza kikao kati yake na Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Eunje Ahn, kuhusu kuimarisha ushirikiano wa maendeleo kati ya mataifa hayo mawili, kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Eunje Ahn, akiahidi kuendeleza ushirikiano wa kimkakati katika nyanja za maendeleo, wakati wa kikao na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akiipongeza Korea Kusini kwa mchango wake katika sekta za maendeleo nchini, wakati wa kikao na Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Eunje Ahn, kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam.
………..
Na. Josephine Majura na Peter Haule, WF, Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, amesema kuwa Serikali ya Tanzania inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa Korea Kusini katika sekta mbalimbali, kupitia nafasi yake kama mshirika wa maendeleo na rafiki wa karibu.
Dkt. Mwamba amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Eunje Ahn, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jjini Dar es Salaam, ambapo mazungumzo hayo yalihusu namna ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa maendeleo kati ya mataifa hayo mawili.
Aidha, aliishukuru Serikali ya Korea Kusini kwa msaada wa kifedha kupitia mikopo nafuu na ruzuku, ambazo zimekuwa chachu ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu na maendeleo nchini.
Katika mazungumzo hayo, Dkt. Mwamba pia alitoa salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kuimarisha zaidi ushirikiano wa pande mbili kwa manufaa ya wananchi wa mataifa haya mawili.
Kwa upande wake, Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mhe. Eunje Ahn, aliahidi kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika miradi ya kimkakati, ili kuhakikisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi yanapatikana kwa manufaa ya wananchi wa mataifa hayo.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha Bw. Melckzedeck Mbise na mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.





No comments:
Post a Comment