Saturday, February 01, 2025

Rais Samia Azindua Sera ya Elimu na Kukabidhi Mobile Clinic

  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini bango maalum lenye ujumbe kuhusu Elimu mara baada ya kukagua mabanda ya maonesho ya masuala ya Elimu katika viwanja vya ukumbi wa mikutano ya Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua mabanda ya maonesho kuhusu masuala mbalimbali ya Elimu kabla ya kuzindua Sera ya Elimu na Mafunzo kwa mwaka 2014, toleo la 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa kampuni ya SC Johnson Family Dkt. Fisk Johnson kutoka Marekani pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma leo tarehe 1 Februari, 2025.
Matukio mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo kwa mwaka 2014, toleo la 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025.



Matukio mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo kwa mwaka 2014, toleo la 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma tarehe 01 Februari, 2025.

Dodoma, 1 Februari 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo ameshiriki katika hafla muhimu zilizofanyika jijini Dodoma, ikiwa ni hatua nyingine katika kuboresha sekta ya elimu na afya nchini.

Katika tukio la kwanza, Rais Samia amekabidhi magari ya huduma ya afya inayotembea (Mobile Clinic) kwa Wilaya za Sikonge na Uyui, mkoani Tabora. Magari hayo yametolewa na Jakaya Kikwete Foundation kwa ufadhili wa kampuni ya SC Johnson Family ya Marekani. 

Hafla hiyo imefanyika Ikulu Chamwino, ambapo Rais Samia amepiga picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa SC Johnson Family, Dkt. Fisk Johnson, pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Baadaye, katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, Rais Samia amezindua rasmi Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023. 

Kabla ya uzinduzi huo, alitembelea mabanda ya maonesho kuhusu masuala mbalimbali ya elimu na kusaini bango maalum lenye ujumbe kuhusu sekta hiyo.

Hafla hii imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wadau wa elimu na maendeleo, pamoja na wananchi waliojitokeza kushuhudia hatua hii muhimu katika mageuzi ya elimu nchini.


No comments:

CCM ARUSHA WAUNGA MKONO AZIMIO, RAIS SAMIA NA RAIS MWINYI WAGOMBEA PEKEE 2025

  Na Vero Ignatus,Arusha MAELFU ya Wananchi wa Mkoa wa Arusha leo Jumamosi Februari 1, 2025 wamejitokeza kwa wingi kwenye tukio la kuung...