Saturday, February 01, 2025

Rais Samia Akabidhi Mobile Clinic kwa Sikonge na Uyui






Dodoma, 1 Februari 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Matiku Chacha, mfano wa ufunguo wa magari maalum ya huduma ya afya inayotembea (Mobile Clinic) kwa ajili ya Wilaya za Sikonge na Uyui.

Magari hayo yametolewa na Jakaya Kikwete Foundation kwa ufadhili wa Kampuni ya SC Johnson Family ya Marekani, ikiwa ni juhudi za kuboresha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa maeneo husika. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

No comments:

SAMIA AZINDUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA WFNS, ATEMBELEA MAONESHO YA SEKTA YA AFYA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitembelea mabanda ya maonesho ya wadau wa Sekta ya Afya kabla ya k...