Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii
imevunja rekodi kwa kufikisha watalii milioni 5.3 (5,360,247) ambapo
idadi ya watalii wa kimataifa 2,141,895 na watalii wa ndani 3,218,352
sawa na lengo lililojiwekea la kufikisha watalii milioni 5 ifikapo 2025.
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi
Chana (Mb) katika hafla ya kutangaza mafanikio katika sekta ya
utalii,iliyofanyika jijini Dar es salaam, tarehe 31 Januari, 2025.
“Ninatoa
shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maono yake makubwa na uongozi wake
thabiti uliotuwezesha kufikia hatua hii. Kupitia jitihada zake, Tanzania
imepata nafasi kubwa zaidi kwenye ramani ya utalii duniani, na tunazidi
kuona matunda ya kazi hiyo kila siku” amesisitiza Mhe. Chana.
Aidha,
ameweka bayana kuwa bado Wizara yake ina wajibu wa kuifikisha Sekta ya
Utalii katika viwango vya juu zaidi ili kustahimili ushindani katika
soko la Kimataifa na kwamba Serikali itaendelea kushirikiana na wadau
wote wa sekta hiyo kuhakikisha inaendelea kuimarisha huduma, kuboresha
miundombinu, na kupanua masoko ya utalii ili Tanzania izidi kuwa kivutio
kinachopendwa zaidi duniani.
“Kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, nawapongeza na kuwashukuru wote mliochangia
mafanikio haya. Kazi yenu ni ya thamani kubwa, na tutaendelea kufanya
kazi pamoja ili kuhakikisha mafanikio haya yanazidi kuimarika mwaka hadi
mwaka” amesema Mhe. Chana.
Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava ameipongeza
Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuwa na utashi wa kisiasa
katika kuiendeleza Sekta ya Utalii.
"Pamoja na kazi kubwa
mnayoifanya na kufika malengo ya ilani ni jambo kubwa sana lakini bado
tuna kazi ta kufikia malengo kwenye mapato tuko bilioni 4 na malengo ni
bilioni 6" amesema Mhe. Mnzava.
Katibu Mkuu wa Maliasili na
Utalii, Dkt.Hassan Abbasi amesema Wizara imejipanga kimkakati
kuhakikisha kuwa inatimiza lengo la makusanyo ya dola bilioni sita za
kimarekani na kuzidi ifikapo Desemba mwaka huu.
Hafla hiyo
imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Maliasili na
Utalii, Taasisi za Serikali, Mashirika binafsi na wadau wa utalii.
Saturday, February 01, 2025
Tanzania Yajivunia Mafanikio Makubwa Katika Sekta ya Utalii
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
CCM ARUSHA WAUNGA MKONO AZIMIO, RAIS SAMIA NA RAIS MWINYI WAGOMBEA PEKEE 2025
Na Vero Ignatus,Arusha MAELFU ya Wananchi wa Mkoa wa Arusha leo Jumamosi Februari 1, 2025 wamejitokeza kwa wingi kwenye tukio la kuung...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
No comments:
Post a Comment