Barua ya wazi kwa Marais Kikwete, Kagame na Kaguta juu ya hali ya Wakenya
Ninashindwa kuwasalimia kwa kheri za mwaka mpya. Katika eneo letu hili la Afrika, hakuna heri, kuna shari tu. Waafrika wenzetu huko Kenya wanakufa bila sababu. Sababu ni moja tu – uchu wa madaraka. Inanishangaza sana kwamba nyie kama viongozi wa nchi za Afrika zinazoshirikiana katika Jumuiya ya Afrika Mashariki yenye lengo la kujenga msingi wa Shirikisho la Afrika, mko kimya. Huu sio wakati wa kucheza mchezo wa kidiplomasia.
Hatutaki, hatutaki kabisa kuona tena jangwa la maauaji ya halaiki yatokee barani Afrika. Tumechoka kuona wanaadamu, Waafrika wenzetu, wakiuawa kama wanyama mitaani na hao wanaojiita eti vyombo vya usalama. Usalama wa nani kama sio wa wananchi?
Jukumu la awali kabisa la vyombo hivyo ni kulinda usalama wa raia; kutuliza ghasia sio kuchochea ghasia au chuki. Wakiwakuta waandamaji bila silaha wawalinde, wawashauri kufanya maandamano yao kwa amani, wawapatie nafasi ya kuonyesha madukuduku yao kuhusu uchaguzi. Bonyeza hapa upate kusoma uchambuzi huu zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
TRC YASAFIRISHA ABIRIA 5,512,995
Shirika la Reli Tanzania (TRC) lilianza kutoa huduma ya usafirishaji abiria kutumia reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) mnamo mwezi Juni...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment