Tuesday, January 01, 2008

Wazungu wamkalia kooni Kibaki

ULE ujanja wa kishetani uliofanywa na Mwai Kibaki, Rais wa Kenya aliyejinyakulia uongozi wa kutangazwa na hatimaye kuapishwa umeanza kumtokea puani baada ya mataifa ya Magharibi kupinga matokeo ya kura za uchaguzi wa Kenya yaliyompa ushindi kuongoza nchi hiyo katika kipindi kingine cha miaka mitano.

Waangalizi wa Kimataifa kutoka Jumuhia ya Ulaya wametoa tamko lao na kuelezea uchaguzi huo ulikuwa na kasoro kubwa.
Waangalizi hao walisema kuwa Rais wa Kenya hakupatikana kihalali na kwamba matokeo hayo hayakukidhi viwango vya kimataifa. Soma habari hii katika shirika la AFP kwa taarifa zaidi.

No comments:

KIKWETE ATEULIWA KUWA MWAKILISHI WA NGAZI YA JUU WA MWENYEKITI WA KAMISHENI YA AU

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AUC), Mhe. Mahmoud Ali Youssouf, amemteua Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Ki...