Saturday, January 19, 2008




Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi ya bweni ya KEMEBOS iliyopo Ijuganyondo katika manispaa ya Bukoba muda mfupi baada ya Rais Kuifungua shule hiyo.




Rais Kikwete akiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Orthodox Tanzania Jeronymos Muzeeyi muda mfupi baada ya Rais kuweka jiwe la msingi katika hospitali hiyo huko Kitendaguro, katika manispaa ya Bukoba, inayojengwa na kanisa hilo eneo la Kitendaguro katika manispaa ya Bukoba jana mchana.

Rais aliushukuru uongozi wa kanisa hilo kwa uamuzi wa kujenga hospitali hiyo Bukoba akisema kuwa itakapokamilika itawapunguzia wakazi wa mji wa Bukoba na maeneo mengine mkoani Kagera adha ya kwenda hospitali ya Rufaa Bugando kwa matibabu ya magonjwa makubwa.

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...