Friday, January 11, 2008

Kenya hakukaliki tena

CHAMA kikuu cha upinzani nchini Kenya cha Orange Democratic Movement (ODM), kimepanga kufanya maandamano makubwa ya siku tatu mfululizo kupinga matokeo yaliyomtangaza Rais Mwai Kibaki kuongoza tena katika kipindi kingine cha miaka mitano ijayo.

Tangazo hilo linafuatia juhudi za kimataifa za kutaka suluhu baina ya pande mbili zinazovutana zilizofanywa na Mwenyekiti wa Muungano wa Afrika (AU), ambaye ni Rais wa Ghana, John Kufuor kushindikana.

Raisi Kufuor aliondoka mjini Nairobi juzi huku akishindwa kukutana na kufanya mazungumzo hayo ya kuleta amani baina ya Raila Odinga na Rais Mwai Kibaki.

Mpaka sasa zaidi ya watu wanaokadiriwa kufikia 600 wameripotiwa kupoteza maisha katika ghasia hizo zilizotokea katika sehemu mbalimbali ya nchi hiyo.

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...