Tuesday, May 24, 2016

ALIYEKUWA MKURUGENZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM AAGWA

Baadhi ya Mawakili na Wanasheria wakiingiza mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bwa. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho.(PICHA NA BEATRICE LYIMO-MAELEZO).
Familia ya aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe wakifuatilia ibada ya kutoa heshima za mwisho ya kuuaga mwili huo.
Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene akiwakisha salamu za rambirambi kutoka Serikalini wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee, leo jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaa Paul Makonda akiwasilisha salamu za rambirambi kutoka ofisi ya Mkuu mkoa wa Dar es salaam wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee, leo jijini Dar es salaam
Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.

No comments:

WAZIRI WA FEDHA: BAJETI YA 2026/27 KUIJENGA TANZANIA YA DIRA YA 2050

  Na Eva Valerian, WF, Dodoma Serikali imesema Bajeti Kuu ya mwaka wa fedha 2026/27 ni ya kipekee kwa kuwa ndiyo bajeti ya kwanza itakayot...