Sunday, June 29, 2025

 









Leo Tarehe 29 Juni, 2025 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Said Shaib Mussa amempokea Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Mhe. Abdisalam Abdi Ali ambaye amewasili leo nchini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Mhe. Abdisalam Abdi Ali anataarijia kuhudhuria maadhimisho ya miaka 65 ya Uhuru wa Somalia ambayo Mgeni rasmi ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.)

Pamoja na Mambo Mengine, Mhe. Abdi Ali anatarajiwa kushiriki mazungumzo ya Uwili kwa ajili ya kujadili na kuibua maeneo mapya ya ushirikiano kati ya mataifa haya mawili na kutembelea Mbuga ya Wanyama ya Mikumi iliyopo Mkoa wa Morogoro.

Tanzania na Jamhuri ya Shirikisho la Somalia ni marafiki wa muda mrefu

No comments:

NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO

  Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Afisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu we...