KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-Moon atatembelea Tanzania baadaye mwezi huu, imethibitishwa mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Ban Ki-Moon amethibtisha mwenyewe kuhusu ziara hiyo ya siku mbili, kuanzia Februari 25, mwaka huu.
Katibu Mkuu huyo alitangaza ziara hiyo wakati alipokutana na kuzungumza na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, katika Kituo cha Mikutano cha UNCC-ECA mjini Addis Ababa.
Viongozi hao wawili wako mjini Addis Ababa, Ethiopia, kuhudhuria mkutano wa 12 wa kawaida wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU).
Ban Ki-Moon alisema atazuru Tanzania baada ya kumaliza ziara yake nchini Afrika Kusini.
Hii itakuwa ziara ya kwanza kwa Katibu mkuu huyo wa UN, kutembelea Tanzania.
Katika mazungumzo hayo, Ki-Moon, alimsifia Naibu Katibu Mkuu wa UN, Dk Asha Rose Migiro wa Tanzania, kwa kuwa mwanamke mchapa kazi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Ziara za Viongozi na Taasisi za Umma Zapamba Moto Tarangire, TANAPA Yafaidi Ongezeko la Watalii wa Ndani
Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) linaendelea kunufaika na mwamko mkubwa wa watalii wa ndani, hususan kupitia safari za mafunzo...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment