Friday, December 28, 2012

Waziri Dk. Fenella Mukangara Amtembelea RC Kanali Mstaafu Fabian Massawe


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kulia) akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera  Kanali Mstaafu Fabian Massawe mara baada ya kumtembelea ofisini kwake jana mjini Bukoba. Waziri Dk. Mukangara yupo mkoani humo kwa ajili ya kuangalia jinsi  fedha za mkopo kutoka mfuko wa vijana  zilivyoweza kuwasaidia vijana kujikwamua kimaisha.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kushoto) akimsikiliza  Mkuu wa Mkoa wa Kagera  Kanali Mstaafu Fabian Massawe alipomtembelea ofisini kwake jana mjini Bukoba. Waziri Dk. Mukangara yupo mkoani humo kwa ajili ya kuangalia jinsi  fedha za mkopo kutoka mfuko wa vijana  zilivyoweza kuwasaidia vijana kujikwamua kimaisha.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kushoto ) akiongea na viongozi wa mkoa wa Kagera (hawapo pichani)jana  mjini Bukoba jinsi  Serikali inavyoangalia uwezekano wa kuongea mkopo kwa SACCOS zinazolenga shughuli za maendeleo ya vijana  kutoka shilingi milioni tano hadi kumi kutokana na mahitaji ya fedha hizo kuwa makubwa. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Vijana James Kajugusi.
Baadhi ya viongozi wa mkoa wa Kagera wakimsikiliza  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (hayupo pichani) wakati akiongea nao kuhusu umuhimu wa kuwafuatilia vijana kwa ukaribu katika Kata na kuweza kuwafundisha na kuwashirikisha  katika miradi ya maendeleo,Picha na Anna Nkinda – Maelezo

No comments: