Leo, Jumatatu tarehe 12 Mei 2025, mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mstaafu), Hayati Cleopa David Msuya, umeendelea kupewa heshima za kitaifa kwa kuwasili rasmi katika Viwanja vya Cleopa David Msuya, vilivyopo Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.
Mapokezi ya mwili huo yamefanyika kwa utulivu na heshima kubwa, yakihudhuriwa na viongozi wa Serikali, viongozi wa dini, familia ya marehemu, pamoja na mamia ya wananchi waliokusanyika kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho kwa mzalendo huyu aliyelitumikia Taifa kwa moyo wa dhati na hekima ya kipekee.
Hayati Msuya ataendelea kukumbukwa kama kiongozi thabiti, mwenye busara, ambaye mchango wake katika ujenzi wa Taifa la Tanzania hauwezi kufutika. Maisha yake ni alama ya utumishi uliotukuka, uadilifu, na uzalendo wa kweli kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
π Ratiba ya maziko na shughuli nyingine za kuaga itaendelea kutolewa na Serikali kupitia vyombo rasmi vya mawasiliano.
π️ Mungu ailaze roho ya Hayati Cleopa David Msuya mahali pema peponi. Amina.
No comments:
Post a Comment