Friday, September 15, 2017

UHAMIAJI YAPATA MSAADA WA VITENDEA KAZI TOKA SHIRIKA LA IOM

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala akipokea msaada wa vifaa mbalimbali uliotolewa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM. Anayekabidhi vifaa hivyo ni, Mwakilishi wa Shirika hilo nchini Tanzania Dkt. Qassim Sufi. Vifaa hivyo vinajumuisha Kompyuta, mashine za kutolea nakala na kuchapishia vyenye thamani ya Dola za Kimarekani elfu arobaini.

Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na wana habari Limefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, Dar es Salaam. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala akibadilishana nyaraka za makabidhiano ya msaada wa vifaa mbalimbali uliotolewa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM. Anayebadilishana naye ni Mwakilishi wa Shirika hilo nchini Tanzania Dkt. Qassim Sufi. Vifaa hivyo vinajumuisha Kompyuta, mashine za kutolea nakala na kuchapishia vyenye thamani ya Dola za Kimarekani elfu arobaini. Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na wanahabari Limefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Makao Makuu yaUhamiaji, Kurasini, Dar es Salaam.

No comments:

MAJALIWA: FANYENI TAFITI ZENYE TIJA KWA WANANCHI

Dar es Salaam, 18 Juni 2025 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa watafiti na wapangaji wa s...