Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe 
(kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliyokuwa ikipigwa na Kikundi 
cha Sanaa na Utamaduni Tanzania (TaSUBA) katika banda lao wakati wa 
Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika 
mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe 
(kushoto) akimsikiliza mjasiriamali wa Tanzania kuhusu baadhi ya bidhaa 
zilizopo katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika
 Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 
2017.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe 
(kulia) akipokea zawadi ya shati toka kwa mjasiriamali wa Tanzania mara 
alipotembelea banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika 
Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 
2017.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe 
(mwenye tai nyekundu) akiangalia moja ya ubunifu wa picha iliyochongwa 
na mjasiriamali wa Tanzania wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa 
Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 
Septemba, 2017.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe 
amewapongeza Wajasiriamali wa Tanzania kwa ushiriki wao katika Tamasha 
la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST.
Dkt.
 Mwakyembe ametoa pongezi hizo leo mjini Kampala nchini Uganda katika 
viwanja vya Mashujaa Kololo alipotembelea kujionea namna tamasha hilo 
lilivyopokelewa na wadau wake walioiwakilisha Tanzania wakiwemo 
wajasiriamali toka vikundi mbalimbali, vikundi vya ngoma, vikundi vya 
sanaa ya maigizo pamoja na baadhi ya wasanii.
Katika
 tamasha hilo, Dkt. Mwakyembe pia alipata fursa ya kutembelea baadhi ya 
mabanda ya wajasiriamali hao pamoja na kuongea nao huku akijionea bidhaa
 mbalimbali zinazouzwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki 
jambo ambalo limemfurahisha sana hususani kwa upande wa watu kutoka 
Tanzania kwakuwa wamejaza mabanda yao kwa bidhaa kadha wa kadha.
“Tamasha
 hili linaonyesha utajiri mkubwa wa sanaa, utamaduni pamoja na bidhaa 
tulizonazo kama nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, na hapa 
tumekutana kwasababu tunabadilishana mawazo na kuonyeshana bidhaa 
mbalimbali za nchi zetu”, alisema Dkt. Mwakyembe.
Aidha,
 katika ziara hiyo, Dkt. Mwakyembe amewatoa wasiwasi wajasiriamali hao 
kuhusu suala la upatikanaji wa masoko huku akiwaahidi kuwatafutia fursa 
ya kuwapeleka wajasiriamali hao pamoja na bidhaa zao Bungeni mjini 
Dodoma ili ziweze kupata soko kwa urahisi kupitia wabunge.
“Niwatoe
 wasiwasi wajasiriamali wote wa Tanzania mliohudhuria hapa, 
nitahakikisha kuwa pindi tunaporudi nyumbani nitatafuta wasaa wa 
kulishawishi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili nyie mpate 
nafasi ya kuleta bidhaa zenu katika viwanja vya Bunge ili basi Wabunge 
wapate kujua haswa vitu vizuri mlivyonavyo nah ii itawasaidia kuviuza 
kwa urahisi zaidi na kujipatia vipato vyenu”, aliongeza Dkt. Mwakyembe.
Sambamba
 na hilo, Dkt, Mwakyembe amewahakikishia wajasiriamali hao kuhusu suala 
la kujitangaza kupitia vyombo vya habari akisema kwamba, atajitahidi 
kutoa ushawishi kwa vyombo vya habari nchini ili viweze kuwapatia muda 
wa kuwatangaza wajasiriamali hao ili wapate kujulikana ikiwemo shughuli 
wazifanyazo.
“Nitahakikisha
 kuwa siku mnapopewa nafasi ya kuja viwanja vya Bunge basi mnapata muda 
wa kutosha katika vyombo vya habari ili mpate kujulikana, hivyo kila 
mmoja wenu naamini atapewa nafasi ya kufanya mahojiano kwa kujieleza 
shughuli azifanyazo na mahali anapopatikana na hii itawasaidia kupata 
masoko zaidi toka kwa watu mbalimbali”, alisema Dkt. Mwakyembe.
Kwa
 upande wao wajasiriamali hao wameshukuru Waziri Mwakyembe kwa juhudi 
alizowafanyia hususani za kuhakikisha kwamba wanahudhuria kwa kiwango 
kikubwa katika tamasha hilo, lakini pia ahadi aliyowapa ya kuwapeleka 
Bungeni ili wakatangaze bidhaa zao na kuwatangaza katika vyombo vya 
habari nchini.
Tamasha
 la JAMAFEST lilianzishwa mwaka 2013 nchini Rwanda na baadhi ya Viongozi
 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kwa mwaka huu tamasha hilo 
linafanyika mjini Kampala nchini Uganda ambapo pia tamasha hili 
linatarajiwa kufanyika tena katika moja ya nchi mwanachama wa Jumuiya ya
 Afrika Mashariki (EAC) mwaka 2019.

 
 
No comments:
Post a Comment