Thursday, November 29, 2012

Waziri Tibaijuka azindua rasmi majengo ya NHC Mchikichini

Majengo ya nyumba za makazi za NHC Mchikichini yakiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi, yatakapokamilika yatakaliwa na familia 48, ambapo katika kila nyumba ina vyumba vitatu jiko na choo pamoja na parking ya kutosha.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa ujenzi wa nyumba 48 za kuuza za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala Mchikichini, Dar es Salaam jana.Anayeongoza kupiga makofi kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akizindua rasmi Ujenzi wa Nyumba za Makazi za  NHC Mchikichini Jijini Dar es Salaam kwa kuweka jiwe la msingi katika katika mojawapo ya majengo ya majengo hayo ikiwa ni mojawapo ya maadhimisho ya miaka hamsini ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) , baada ya uwekaji wa jiwe la msingi alikagua ujenzi wa mradi huo wa nyumba.
 
Msondo Ngoma walikuwapo kwenye uzinduzi wa nyumba za makazi za Mchikichini
Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu akizungumza na MC maarufu nchini na Mtangazaji wa Kipindi cha Maisha ni Nyumba, Ephraim Kibonde (picha ya juu) pamoja na mtangazaji wa TBC (picha ya chini) baada ya uzinduzi  rasmi wa Ujenzi wa Nyumba za Makazi za  NHC Mchikichini Jijini Dar es Salaam ikiwa ni mojawapo ya maadhimisho ya miaka hamsini ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) , baada ya uwekaji wa jiwe la msingi alikagua ujenzi wa mradi huo wa nyumba.

No comments: