Tuesday, November 06, 2012

Breaking News: Mhashamu Askofu Alosius Balina afariki dunia

MHASHAMU Askofu mkuu wa Jimbo la Shinyanga Kanisa katoliki amefariki dunia akiwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando alikokuwa akitibiwa.
  
Historia yake:
Mhashamu Askofu Aloysius Balina alizaliwa Juni 21, 1945 katika kijiji cha Isoso Ntuzu wilayani Bariadi  mkoani Shinyanga na aliwekwa wakfu na Papa Yohane Paulo II mwaka 1984 kuwa Askofu wa Geita na kusimikwa Machi 10, 1985.
Septemba 23, 1997 alihamishiwa Jimbo la Shinyanga na kuwa Akofu wa tatu wa Jimbo la Shinyanga hadi mauti yalipomkuta, huku watangulizi wake wakiwa Askofu Edward A. McGurkin, aliyetumikia cheo hicho toka mwaka 1956 hadi 1975, alifariki Agost 281983 huko Marekani, wa pili ni Askofu Castor Sekwa, aliyetumikiwa kuaznia mwaka 1975  hadi  Juzi 6, 1996 alippofariki na askofu Balina kushika nafasi yake.

Taarifa kamili zitatolewa baadaye 
                     *******************************
21 Jun 1945 Born - Isoso Village
27 Jun 1971 Ordained Priest - Priest of Shinyanga, Tanzania
8 Nov 1984 Appointed - Bishop of Geita, Tanzania
6 Jan 1985 Ordained Bishop - Bishop of Geita, Tanzania
8 Aug 1997 Appointed - Bishop of Shinyanga, Tanzania 


HABARI KWA MUJIBU WA BLOGU YA Katulanda News

No comments: