Sunday, November 25, 2012

KINANA, NAPE, KHATIB WAFUNIKA JIJINI ARUSHA

Kinana akisalimiana na Lowassa katika Uwanja wa Ndege wa Arusha. Kushoto ni Katibu wa CCM Arusha, Mary Chatanda.
 
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akisalimiana na Lowassa Uwanja wa Ndege wa Arusha. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda.
 
Pikipiki zikiongoza msafara wa Kinana, kutoka Uwanja wa Ndege wa Arusha.
 
Kinana akifungua shina la wakereketwa wajasiriamali wa CCM Tawi la Nguruma, Arumeru, Arusha jana.
 
Ngoma ya Kimasai wakati wa mkutano wa Meru, jijini Arusha jana.
 
Kinana akisalimia wananchi baada ya kuwasili Uwanja wa Usa River kuhutubia mkutano wa hadhara.
 
Nape akizungumza jambo la Lowassa kwenye mkutano wa Kinana uliofanyika Usa River, Arusha.
 
Baadhi ya vijana 150 wa Chadema waliohamia CCM wakionyesha kadi za Chadema, wakati wa mkutano wa Usa River jana.
 
Wazee wa Kimeru, wakimkabidhi vitendea kazi vya jadi, Katibu Mkuu wa CCM, Kinana katika mkutano uliofanyika Usa River, Arusha. Anayemkabidhi ni Ezrom Sumari.
 
Kinana akivishwa mavazi ya jadi ya Wameru wakati wa mkutano uliofanyika Usa River, Arusha jana.
 
Mzee Willson Meng'atu akimvisha vazi la heshima Nape Nnauye kama ishara ya wazee wa Kimeru kutambua upambanaji wake katika kujenga Chama, wakati wa mkutano wa Usa River, Arusha jana.
 
Wazee wa Kimeru wakimvisha vazi la jadi, Katibu wa NEC Oganaizesheni, Mohamed Seif Khatib kumpongeza kushika nafasi hiyo ya kujenga uhai wa Chama, kwenye mkutano wa CCM Usa River, Arusha jana.
(Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments: