BENKI YA TIB YATENGA BILIONI 30 KWA AJILI YA KUKOPESHA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara Kutoka Benki ya TIB  Joseph Chilambo akizungumza na Wajasiriamali katika Mkutano uliondaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake (TWCC) Jijini Dar es Salaam
Wanawake Wafanyabiashara waliojitokeza katika Mkutano wa Mwezi Kwa Wafanyabiashara Wanawake na  Kundi la Vijana ulioandaliwa na Chama cha  Wafanyabiashara Wanawake nchini (TWCC) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam

Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara wa Benki ya TIB Joseph Chilambo  akisikiliza Kwa Makini Mawazo yanaowasilishwa na Wafanyabiashara Wanawake na Vijana katika Mkutano wa Mwezi uliondaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake (TWCC) uliowakutanisha Watoa huduma kwa Wajasiriamali wakubwa na wadogo Jijini Dar es Salaam

BENKI ya Maendeleo ya TIB ilishiriki katika mkutano wa kifungua kinywa wa Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) uliowakutanisha Wajasiriamali wanawake kutoka mikoa yote ya Tanzania.

Hafla hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, ilitoa jukwaa muhimu kwa wanawake kuweka mtandao na kuongeza uelewa kuhusu fursa mbalimbali za biashara na fedha.

Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara wa TIB Joseph Chilambo aliwasilisha huduma mbalimbali za fedha za uwekezaji ambazo benki hiyo inatoa wanawake wanaomiliki biashara ndogo na za kati. Bw. Chilambo alisisitiza kujitolea kwa benki hiyo kwa makampuni ya biashara yanayomilikiwa na wanawake .

"Kusaidia SMEs ndio msingi wa majukumu yetu, ndiyo maana tunajivunia kuunga mkono mpango huu muhimu kwa SME zinazoongozwa na wanawake.

Hizi ni pamoja na vifurushi vya mkopo vinavyobadilika, programu za kujenga uwezo, na huduma za ushauri zinazolenga kuimarisha ukuaji wa biashara na uendelevu.

Benki inasalia kujitolea kukuza ukuaji, kuimarisha biashara zinazomilikiwa na wanawake, na kuendeleza uwezeshaji wa kiuchumi kote nchini.

Hata hivyo amesema Benki hiyo imeweka Kiasi cha Shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya Wajasiriamali Wanawake Kukopeshwa ili kukuza mitaji yao ya Biashara.

Pia amesihi Wanaotaka Kufungua Viwanda na Biashara kubwa kuweza kufika katika Benki hiyo huku vigezo kikubwa ili aweze kukopeshwa ni pamoja na Biashara hiyo iwe Imesajiliwa na cheti cha Brela na Mradi ambao umeandikiwa mpango wa Biashara hiyo.

Huku mrejesho wa mkopo huo unaweza kuwa kwa Mwezi au Mwaka kulingana na Biashara yenyewe na namna fedha inayoingia kupitia biashara hiyo huku Wafanyabiashara wadogo na Wakubwa wanaweza kukopesheka.

Ametoa wito kwa Wafanyabiashara kujitahidi kutunza hesabu za kibiashara ili Benki inayowakopesha iwe rahisi kuwa na Taarifa sahihi ya Kiwango kinachoingiza kupitia biashara hiyo.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wafanyabiashara Wanawake nchini (TWCC) Mwajuma Hamza amesema Mkutano huo mahususi kuwakutanisha Wajasiriamali pamoja na Wadau wa Biashara ili kurahisisha mifumo ya utunzaji fedha pamoja na Kukuza Mitaji kwa Wajasiriamali wadogo na Wakati.

Hata hivyo ameongeza kuwa Watoa Huduma kupitia Mkutano huo wataweza kujua pesa zinazotengwa kwa ajili ya kuwakopesha Wajasiriamali hao ziongezwe Kutokana na ukubwa wa Biashara zao.

Pia ametoa wito kwa Wajasiriamali Wanawake waweze kutambulika kisheria biashara zao,kukuza Majina yao pamoja na kupata tenda za serikalini kwani Chama hicho kinawapa fursa Wanawake kushirki Mikutano mbalimbali inayoandaliwa nchi nzima lengo ni kuwakutanisha Wanawake Wajasiriamali wote kutambulika na Kupata Mikopo ya Kibenki kiurahisi.

Comments